Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niseme machache katika bajeti hii. Kwanza nianze kwa kuwapongeza Waheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya katika kutekeleza majukumu yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwaambia kwamba, tunatekeleza bajeti kulingana na mapato tunayoyapata. Pia lazima tufahamu kwamba katika uchumi tunafahamu mahitaji ni mengi kuliko rasilimali za kutekeleza mahitaji hayo. Kwa hiyo, napenda kusema kwamba uchumi unatufundisha pia kwamba unapokuwa unatenga bajeti, bajeti ni nini? Bajeti is an intelligent guess.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, unaweza kufikiria na ku-plan mipango yako, lakini unapoendelea kuitekeleza bajeti hiyo yapo mengine ya msingi yanayo-emerge na unaweza kuyatekeleza. Ndiyo maana hata Sheria ya Bajeti imetoa nafasi hiyo kwamba, yapo mengine yanayotokea na unaweza kuyatekeleza, lakini ukiwa ndani ya wigo ule wa bajeti ambayo imepitishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti zilizotekelezwa hakuna jambo lolote lililotekelezwa nje ya bajeti ambayo tumeipitisha. Pia, nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba, Sheria yetu ya Bajeti, Kifungu cha 41 na Kanuni ya 28 ya Sheria hii ya Bajeti, Namba 11 imempa nafasi Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango kuweza kuhamisha fedha kutoka katika Vote moja kwenda Vote nyingine katika utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali yetu pia inawasilisha Bungeni Taarifa za kuhamisha matumizi hayo kutoka Vote moja kwenda Vote nyingine na nirudie kusema kwamba, hakuna sehemu ambako tumevuka pale ambapo bajeti yetu ya Serikali tulikuwa tumeipitisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee jambo moja ambalo limesemwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwamba, ili kutekeleza majukumu yake wamependekeza, Tume ya Pamoja ya Fedha iweze kutekeleza majukumu yake chini ya Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais. Katika hili naomba niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwamba, ni muhimu tukaenda katika majukumu ya Tume hii ya Pamoja, majukumu yake ni yapi, ina-deal na mapato kutoka pande zote za Muungano na ndiyo maana ikawekwa chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume hii ya Pamoja imefanya ziara katika nchi mbalimbali zenye mfumo huu kama nchi yetu ya Muungano au Shirikisho, kote walikokwenda wamekwenda zaidi ya nchi tisa. Katika nchi hizi ni nchi tatu tu ambazo Tume hii ya Pamoja ya Fedha haiko chini ya Wizara ya Fedha na Mipango, kama ambavyo nimesema turejee kwenye majukumu ya Tume hii kabla hatujapendekeza jambo lingine ili kuweza kuhakikisha kwamba, Tume inafanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kulizungumzia jambo la corporate tax. Jambo la corporate tax lipo kisheria na linatekelezwa kwa Sheria yetu ya Mapato na naomba nilikumbushe Bunge lako Tukufu kwamba, kama alivyosema mchangiaji makampuni hulipa corporate tax kule yalikosajiliwa, lakini tunapoweza kutoa hoja zetu pia tufikirie na tuangalie manufaa ya hiki tunachokipendekeza.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.