Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema. Naanza kwa kuchangia Wizara hii ambayo inahusiana na Katiba na Sheria ambavyo vyote ndio msingi wa haki. Mfano; katika kitabu cha Hotuba ukurasa wa 36 kipengele cha Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora:-
(i) Kukuza na kutetea haki za binadamu hususan makundi yenye mahitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maneno haya yameandikwa lakini hayafanyiwi kazi na ushahidi kuna mahabusu na wafungwa wengi ambao wamefungwa bila kupatiwa haki za kisheria kwa kutetewa na wanasheria wa Serikali, kutojua haki zao lakini pia kwa kesi za kubambikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo akinamama wajawazito wanaojifungulia Magerezani na pia wapo wanaotiwa hatiani wakiwa na watoto wachanga ambao bado wananyonya maziwa ya mama zao na hawawezi kuishi bila ya mama zao, wanakuwa wafungwa bila hatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu; Serikali itafute adhabu mbadala kuwaepusha watoto kuwa wafungwa bila hatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Katiba na Sheria nimeishangaa kwa kutoweka katika Bajeti yake Fungu la Fedha kwa ajili ya kuendeleza mjadala wa Katiba mpya ambayo ndio haja ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria itenge fedha kwa ajili ya mwendelezo wa mjadala wa Katiba mpya ili kuondoa kiu ya Katiba mpya kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakimu kukaa katika Vituo vyao kwa muda mrefu wanazoeleka na wanazoea na kuwa wepesi kuweza kupokea rushwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakimu waongezewe mishahara ili kuwaepusha katika suala zima la kupokea rushwa.