Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kazi nzuri inayofanywa. Pamoja na kuwepo changamoto ya umuhimu wa kuboresha baadhi ya sheria ambazo ama zimepitwa na wakati au zinahitaji kuweka mkazo/udhibiti katika baadhi ya maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma hotuba hii kikamilifu na kubaini kuwa ahadi iliyotolewa Bungeni na Waziri mtangulizi kuhusu Wilaya mpya ya Mkalama kutokuwa na Mahakama ya Wilaya ilihali wananchi wakiifuata haki Wilaya ya Iramba Magharibi. Wakati jibu likitolewa katika swali la msingi lililoulizwa na Mbunge wa Iramba Mashariki Mheshimiwa Allan Kiula iliahidiwa kuwa bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha 2017/2018 itaweka/itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Mkalama lakini sijaona utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara itenge fedha katika bajeti hii ili kuwasaidia wananchi wa Mkalama ambao wamewekwa wakihangaika kupata haki katika Wilaya nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naunga mkono hoja.