Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katiba mpya, Wizara haina muda tena wa kusubiri kuanza kumalizia mchakato wa kupata katiba mpya. Kama bajeti hii ya 2017/2018 haitatenga pesa kwa ajili ya jambo hili, maana yake Watanzania wasitegemee tena kupata katiba mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, marekebisho ya sheria, Serikali ilete Muswada Bungeni kwa ajili ya kubadilisha sheria ya mabadiliko ya katiba ya 2011 na ile ya kura ya maoni ya 3013 ili iendane na hali ya sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zuio la shughuli za kisiasa, Serikali itengue zuio lake la kuwakataza wanasiasa kufanya mikutano ya kisiasa kwani kwa kufanya hivyo inavunja sheria ya vyama vya siasa. Ni haki ya msingi ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo chakavu, Wizara itafute vyanzo vyake vingine ili ipate fedha za kujenga na kukarabati majengo ya mahakama hasa Mahakama ya Mwanzo.