Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi ya kuchangia. Ucheleweshwaji wa kusikiliza kesi za mahabusu. Baada ya kesi zilizopo katika uchunguzi chini ya DPP zinachukua muda mrefu sana na wakati watuhumiwa wengine hawana hatia lakini wanaweza kuwa gerezani kwa zaidi ya miezi sita. Je, kesi hizi hazina kikomo cha uchunguzi? Inakuwa kama wanakomoa na kudhalilisha wengine na huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya Mfuko wa Mahakama, bado mfuko huu wa fedha zinazoainishwa hazifiki kwa wakati na hata wakizipata zinakuja zimechelewa na pungufu ambayo inakuwa ni vigumu kutekeleza miradi ya maendeleo hii inajionesha mpaka Machi 2017, fedha hazikutumwa kwa wakati. Chombo hiki ni muhimu sana nashauri fedha zipelekwe kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wapo watumishi wa kutosha, kuhakikisha posho za wazee wa mabaraza zinalipwa, wazee hawa wanaacha shughuli zao wengine inabidi watumie nauli zao, hivyo, wana haki ya kupata stahili zao kwa wakati.