Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Katiba na Sheria ina wajibu wa kuiwezesha nchi kuwa na mfumo mbalimbali wa Kikatiba na Kisheria katika kufanikisha Mipango ya Maendeleo ya Taifa. Pamoja na wajibu huu muhimu hotuba nzima ya Waziri haijazungumzia kabisa kuhusu mchakato wa Katiba mpya. Aidha, katika vitabu vya bajeti hakujatengwa fedha zozote/kiasi chochote kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa Katiba mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali inadhihirisha kwamba Serikali ya Rais Dkt. John Magufuli lazima dhamira ya kuendeleza kwa wakati mchakato wa mabadiliko ya katiba. Hivyo ni vyema Serikali ikatoa kauli hii Bungeni ni kwa nini haijatenga fedha kwa ajili ya mchakato huu muhimu kwa maslahi ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika aya ya 20, 21, 22, Waziri wa Katiba na Sheria amezungumzia kuhusu utekelezaji wa mkakati wa kuboresha huduma za Mahakama ikiwa ni pamoja na kufanya ujenzi na ukarabati wa Mahakama mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika orodha hiyo imetajwa Wilaya mpya ya Kigamboni, hata hivyo Wilaya mpya ya Ubungo haijatajwa hivyo, Serikali itoe kauli ni kwa nini Wilaya mpya ya Ubungo haijajumuishwa na lini Mahakama ya Wilaya ya Ubungo itajengwa. Aidha, Mahakama hiyo ni vyema ikajengwa katika Jimbo la Kibamba yalipo Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Ubungo kama ilivyopendekezwa kwa nyakati mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume ya kurekebisha Sheria ina wajibu na mpango muhimu ya maboresho ambayo yamependekezwa muda mrefu ni pamoja na matumizi ya lugha ya Kiswahili katika mfumo mzima wa Mahakama na utungaji sheria nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imeeleza kuwa imefanya uchaguzi kuhusu mabadiliko yaliyowasilishwa katika THUB.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiwa Mbunge wa Ubungo niliwasilisha malalamiko na madai ya kutaka, uchunguzi kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu na misingi yake ya utawala bora juu ya mgogoro wa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu matatizo ya maji katika Kata ya Goba naomba kupatiwa majibu juu ya hatua ambazo Tume imechukua na kupatiwa nakala ya ripoti ya Tume kuhusu uchunguzi huo. Aidha pamoja na uwekezaji mkubwa wa Serikali juu ya miradi ya Ruvu juu na Ruvu chini tume ielewe kwamba Goba bado imeachwa kama kisiwa kwa kuwa haina mtaro wa mabomba.