Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuipongeza Serikali na Waziri husika kwa hotuba nzuri inayohusu makadirio na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi zimekuwa mahali muhimu kwa ajili ya kutoa haki katika nchi yetu. Hata hivyo, nimesikitika sana kuona kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 Wizara ilitaja Wilaya 17 zitakazojengwa Mahakama ya Wilaya na moja ya Wilaya hizo ni Kilindi. Naomba kupata majibu ya kuridhisha kwa nini Wilaya ya Kilindi si miongoni mwa Wilaya zilizopo katika ujenzi kwa mwaka huu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni takribani miaka 30 sasa wakazi wa Wilaya ya Kilindi wamekuwa wakipata huduma za Mahakama za Wilaya katika Wilaya jirani ya Handeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upo umbali mrefu sana kutoka Kilindi na Handeni hususani kwa Kata za Pagwi, Kikunde, Tunguli kata hizo zipo karibu kabisa na Wilaya ya Gairo. Utaona kwa kiasi wananchi wa kilindi wanahitaji Mahakama hii kwani kupata Mahakama ni sehemu ya haki za msingi kwa wananchi wa Kilindi. Halmashauri inalo eneo kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Niombe sasa Wizara ione umuhimu wa kuwapatia wananchi Mahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Uhaba wa Mahakama za Mwanzo; Mahakama za Mwanzo pia zimekuwa ni chombo muhimu sana katika kutoa haki kwa wananchi wetu, lakini maeneo mengi hayana Mahakama za Mwanzo na hata kama zipo basi zimechakaa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano katika Jimbo langu la Kilindi yote tarafa nne, kata 21 na vijiji 102 tunazo Mahakama za Mwanzo zisizozidi tano, hali hii ni mbaya sana. Ningeomba kauli ya Wizara na Waziri mwenye dhamana ya Mahakama hizi ni lini watu wa Kilindi watapata Mahakama za Mwanzo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na Mahakama za Mwanzo Kata za Kimbe, Mgora, Kwekiku, lakini Mahakama hizi zote majengo yake yote yamekuwa magofu na hakuna Mahakimu, je, lini Mahakama hizi zitajengwa upya? Niombe Waziri alichukue jambo hili kwa uzito mkubwa unaostahiki
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.