Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kumpongeza Waziri Profesa Kabudi na watendaji wote wa Wizara kwa kutuletea bajeti yao ili tuweze kuijadili. Kuna mambo ambayo nataka kuyapatia ufafanuzi wake na kushauri pia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ucheleweshaji wa kesi za ubakaji; Mkoa wetu wa Iringa ni kati ya mikoa inayokabiliwa na idadi kubwa sana ya kesi ya ubakaji na ulawiti. Inasikitisha sana Bunge lililopita nilileta swali langu hapa Bungeni na niliweza kutoa takwimu ya mwaka 2016 kesi 217 lakini zilizoweza kufikishwa Mahakamani ni kesi 27 tu lakini kila mwaka katika mkoa wetu matukio ya ubakaji yanazidi kuongezeka. Napenda kujua mkakati wa Serikali kuhusiana na jambo hili ni kwa nini kusiwepo na Mahakama Maalum ya kushughulikia kesi hizi. Matukio haya yamekuwa yakiwaathiri watoto wetu kiakili pamoja na mama zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ucheleweshaji wa mabadiliko ya sheria zilizopitwa na wakati; baadhi ya sheria zetu hapa nchini zimekuwa ni za muda mrefu sana na zimepitwa na wakati na kusababisha baadhi ya sheria zetu hapa nchini kutoendana na mabadiliko na kasi ya maendeleo ya Taifa na kuonekana kuwa zimepitwa na wakati. Mara nyingi sana sisi Wabunge tumekuwa tukileta hoja zetu hapa Bungeni lakini bado hatupatiwi majibu ya kuridhisha. Kwa mfano, 12 Aprili, 2017 nilileta swali kuhusiana na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 lakini bado majibu yake hayaridhishi. Je, ni lini sasa Serikali italeta hoja ya kufanya marekebisho ya kuboresha baadhi ya sheria zilizopitwa na wakati?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ufinyu wa bajeti, Wizara hii ni muhimu sana na imekuwa na malalamiko mengi kwa wananchi kutomaliza kesi zao au kuchukua muda mrefu sana. Pia miradi mingi kutokamilika kwa wakati pamoja na bajeti yao kuwa kidogo sana lakini pia pesa yao imekuwa ikicheleweshwa sana na kusababisha miradi kutokamilika kwa wakati hivyo kusababisha miradi hiyo kutumia pesa nyingi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.