Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria


MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono Hoja ya Serikali au Wizara ya Katiba na Sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo malalamiko katika eneo hili la Mahakama. Hatuna Mahakama katika eneo la Haydom ambapo pana watu zaidi ya hamsini elfu na wapo pembezoni na Halmashauri ya Mji wa Mbulu ni kilomita 86 toka Makao Makuu ya Wilaya ambapo ipo Mahakama ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunacho Kituo cha Polisi Haydom ambapo tunaomba tujengewe Mahakama hata ya Mwanzo. Tumekwisha tenga kiwanja cha kujenga Mahakama. Kituo cha Polisi kinafanya kazi ya kukamata wabadhirifu na kuwasafirisha Mbulu zaidi ya kilomita 86 hivyo kuipa Serikali gharama kubwa sana ya kupeleka mahabusu/ watuhumiwa zaidi ya kilometa nilizozitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tujengewe Mahakama Haydom maana wakati mwingine Polisi hutumia mabasi kusafirisha watuhumiwa na wakati mwingine kutoroka na kupotea. Hivyo naomba sana.