Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, usikilizaji wa mashauri mahakamani; pamoja na Serikali kueleza 80% ya mashauri yameweza kusikilizwa, kasi hii bado inahitaji kuwekewa nguvu zaidi ili kuendelea kupunguza mrundikano wa kesi zilizopo mahakamani. Serikali lazima itie nguvu na mkazo katika Mahakama za Mwanzo na Mahakama za Wilaya kwani huko ndiko kwenye mrundikano wa kesi nyingi, jambo ambalo linawafanya wananchi wenye kesi mbalimbali kuendelea kutumia muda mwingi mahakamani. Hata hivyo, haki inayocheleweshwa ni sawa na haki iliyonyimwa. Nashauri Serikali iendelee kujipanga kuhakikisha mrundikano wa kesi katika mahakama za chini zinakwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo; pamoja na umuhimu wa Taasisi hii ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo, ipo haja ya kuongeza chuo hiki katika kanda nyingine za nchi hii. Ni ukweli kuwa nchi hii ni kubwa na wanafunzi wanaohitaji kupata mafunzo haya ni wengi. Hivyo basi, ni muhimu kwa Serikali kuongeza vituo vya mafunzo hayo kwa angalau Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kati, Kusini na Magharibi. Kwa kuongeza vituo hivyo itasaidia wanafunzi kumudu gharama za mafunzo na hivyo kuongeza wanafunzi zaidi.