Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi kuwa mmoja wa wachangiaji katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziiri pamoja na timu yake yote katika Wizara hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, cha pili ni kuhusu barabara zangu za jimbo la Gairo ambayo ni ahadi ya aliyekuwa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ambayo aliitoa tarehe 26 Juni, 2014 tarehe 26. Kwanza ni shukuru, maana usiposhukuru na kidogo basi ujue wewe shukrani huna tu hata ukienda mbinguni huko ni hivyo. Ukiangalia hata kwenye youtube ukiandika tu Magufuli Gairo au Magufuli aitwa jembe Gairo utaona hotuba yake inakuja pale. Alitoa ahadi ya barabara ya kutoka Gairo kwenda Chakwale kwenda Kilindi kwa kiwango cha lami. Alitoa ahadi ya kuweka Mji wa Gairo kilometa 5 za lami Gairo Mjini. Alitoa ahadi ya Gairo - Nongwe kilometa 76 kuchukuliwa au kukasimiwa na TANROADS. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nasema hivyo kwanza na mpongeza Mheshimiwa Rais, na ninamshukuru Mheshimiwa Rais na ninamshukuru Waziri wa ujenzi kwamba; nikiangalia katika hotuba ya kitabu cha Waziri wa Ujenzi ukurasa wa 339 naiona barabara ya Nongwe imetengewa zaidi ya milioni 900 na kwa bahati nzuri mkandarasi wa kuweka lami Gairo Mjini tayari yupo kazini pale na anaendelea kazi ya kuweka zile kilometa tatu za lami.
Nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri, kwamba katika ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kilomita 5 zimebakia kilometa mbili, na wakati Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi anatupa ahadi ya unjezi wa kilometa tano alikuwa anaelewa matatizo yaliyopo pale. Kwa hiyo, tumepewa kilometa tatu lakini tunaomba hizi kilometa mbili zimaliziwe haraka, kwa sababu mwaka huu sijaziona kwenye bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ukiacha hizi kilometa tatu peke yake ni sawa sawa na mtu kumvalisha koti la suti halafu chini umemvalisha kaptula. Kwa hiyo naomba tumalize hizi kilometa mbili. Vilevile nikiangalia ile barabara ya kutoka Gairo kwenda Kilindi kwa ndugu yangu Kigua, ambayo ingesaidia hata watu wanaotoka Iringa kupitia Dodoma, Zambia wapi kwenda bandari ya Tanga kwa sababu pale ni karibu sana kutoka Gairo mpaka Kilindi ni kilometa 100 tu nayo haimo kwenye bajeti. Kwa hiyo na washauri na najua hii Wizara ni sikivu mtaweka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, cha zaidi ambacho nilitaka kukiongea kwa leo ni kuhusu habari ya mashirika ya umma. Watu wengi wamepongeza sana mashirika yote ya umma ambayo yako chini ya Wizara hii ya Ujenzi. Wizara hii ya Ujenzi ni moyo wa nchi, Wizara hii ina taasisi 37, na moja ya hizo Taasisi kubwa nizitaje chache kuna TTCL, Posta, Bandari, ATC, TRA, hizo nikutajie tano ambazo zote ni kubwa kabisa. Nataka niseme kwamba namshukuru Mheshimiwa Rais, nimpongeze pamoja na Mheshimiwa Wazari na Mheshimiwa Naibu Waziri na Makatibu wa Wizara hii wote kwa kupata Bodi ambazo zinaongozwa na watu ambao wana weledi, wajumbe wenye weledi na ma-CEO. Ukichukua taasisi zote nilizozitaja ma-CEO ni vijana na ni wazuri kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, wasiwasi wangu uko wapi? Haya mashirika ambayo yako kwenye hii Wizara ukiangalia sana ya natakiwa yaendee kibiashara. Shirika la Reli lazima liende kibiashara, TTCL lazima iende kibiashara, ATCL lazima iende kibiashara, Posta lazima iendee kibiashara, bandari lazima iendee kibiashara hata Mheshimiwa Rais wakati ananua ndege alijua kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika hakuna watu wanafiki kama baadhi ya sisi Wabunge. Miaka ya juma tunapiga kelele tunafananishwa na Rwanda. Rwanda wana ndege sisi hata kimoja hichi kibovu bovu, leo ndege zimekuja mnaanza kusema ndege sio kipaumbele cha kwanza. Mimi nasema vyote ni vipaumbele, lakini viongozwe kwa mujibu wa sheria za kibiashara, hicho ndio cha msingi. Kwa mfano, unaunda
Bodi, zina madaktari, zina maprofesa zina wajumbe safi halafu baadaye tena hapo hapo yanatoka maagizo, matamko kutoka huku ya naingilia kwenye ile Bodi. Sasa kuna faida gani ya kuweka Bodi mpya? Acheni watu wafanye kwa kutumia utaalamu wao. Kama mmeweka Bodi basi acheni Bodi pamoja na ma-CEO wao na Menejimenti zifanye kazi yake; lakini kutakuwa na faida gani ya kuweka bodi mpya halafu mnaziingilia ingilia? Hii ni biashara jamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni wapeni mfano mmoja hili shirika letu la TTCL; hili ni shirika ambalo lingekuwa linachangia uchumi wa Taifa. Tuchukue mfano wa shirika la simu la Ethopia, kwa mwaka wanatengeneza dola bilioni 3.3, ukitoa kodi wanabaki na dola bilioni 1.5. Kwenye mfuko wa Serikali wanachangia karibu dola milioni 300, hiyo ni sawa sawa na bilioni zaidi ya 700 za Tanzania. Sasa haya sio tunawategemea TRA lazima tuwe na mashirika ambayo yataingiza hela kwenye Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia uwekezaji wa TTCL, ili ifike Tanzania nzima itachukua zaidi ya miaka, na ikimaliza kufika huko vijijini na sehemu nyingine hawa Vodacom na kampuni zingine kama Tigo, watakuwa tayari wana mitandao mipya. Wakati huko huko Serikali tena ina asilimia 40 kwenye Shirika la Airtel, kama Wabunge hawafahamu. Asilimia 40 ya Airtel ni hela ya Serikali ya Tanzania, lakini toka hizo asilimia 40 ziwekwe kwenye Airtel kila siku Airtel wanapata hasara hawaleti faida hata shilingi moja kwenye Serikali. Sasa kwa nini hizo hisa za kwo 60 zilizobakia tusizinunue ziwe za Serikali (TTCL) halafu tutakuwa tayari tumeshajigawanya, tumeshachukua mitambo ya Airtel tunakuwa tayari tuko Tanzania nzima na tunaingia kwenye compentintion? Kuliko kuacha asilimia 40 wakati ilie asilimia 40 kila siku hawapati faida. Kwa hiyo, hela ya Serikali imekaa tu Airtel. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukija kwenye shirika la ndege; uwekezaji wa ndege si mchezo. Ukiwa bilionea ukitaka kuwa milionea ingia kwenye biashara ya ndege. Inataka lazima muwe na mtaji na lazima uweke mtaji.
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Naibu Spika, ila hilo shirika linatakiwa lipewe hela lijiendeshe, TTCL.