Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, na momi nachukua nafasi hii kukushukuru kunipa nafasi, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kwanza nitoe pongezi za dhati kwa Serikali, Mheshimia Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mheshimiwa Waziri mwenye Wizara hii kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. Lazima tuwapongeze sababu Wizara hii imeshika mambo mengi kwenye nchi lakini bado inafanya kazi vizuri sana, lazima tuwape pongezi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mabadiliko makubwa sana yamepatikana kwa kipindi kifupi sana toka Mheshimiwa Rais aingie madarakani na hasa alivyompa Wizara hizi tatu Mheshimiwa Mbarawa. The Country is progressing sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitajikita kwenye maeneo yale ya siku zote, yapo mabadiliko kidogo tumeyaona, lakini Mheshimiwa Waziri nilitaka nikwambie sijui kama ulishawahi kuona kiti kinawahi kukamata mshahara wa Waziri; na Kiti kikikamata mshahara wa Waziri ujue kura ikipigwa ujue Kiti kitasema nini. Haya mambo tunayasema; kuna mtu juzi nimekutana naye anasema wanashukuru Ethiopia imewafungua macho kwenye mambo ya simu. Tumeyasema haya miaka mitano hamjafungua macho? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi na kuomba Mheshimiwa Waziri ni mchapakazi vizuri sana, cash cow ya Tanzania sasa hivi ni Shirika la Simu la TTCL. Kama tumeweza kununua ndege zetu, ni hatua nzuri sana ambayo Serikali imeifanya, ni lazima tui-bail out TTCL ili nayo iweze kutoa mchango mkubwa sana wa GDP kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi wana utawala mpya, kuna CEO mpya kijana, kabobea, taaluma zake anafanya kazi vizuri, Chairman mpya kachaguliwa mzuri, wanachohitaji ni affirmative action ya Serikali katika kuwasaidia. Sasa mimi nakuomba Mheshimiwa Waziri tupate majibu mazuri kuhakikisha TTCL kweli inasaidiwa na Waheshimiwa Wabunge tuwe mabalozi wa TTCL ili tuweze kusaidia Serikali yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, TTCL ni shirika la umma, its high time Serikali ikaipa exclusive rights za TTCL ku-handle masuala yote ya IT Nchi nzima badala ya kutegemea wakandarasi binafsi. Leo Serikali ina-share asilimia 39 mpaka 40 Airtel. Toka Serikali iweke pesa zake Airtel hakuna faida yoyote ambayo imekuwa decrared na Kampuni hii. Kwa nini sasa Serikali isitoe pesa zake ikaziingiza TTCL ili Shirika hili liweze kubobea? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulitoa ushauri hapa kuhusu TCRA sasa wazibane kampuni za simu kwenye correction za kodi za Serikali kwenye VAT na excise-duty ziwe displayed kwenye simu kuonesha kweli kodi ya Serikali inapatikana. Lakini bado napata kigugumizi, hizi display kwenye simu zetu hazina feed kwenda TRA. Kwa hiyo, TRA hawana taarifa ya kodi inayokusanywa, huyu mkandarasi ambaye aliyepewa kazi hii ya TTMS there is something wrong with this thing.

Mheshimiwa Naibu Spika, mtambo huu ni mali ya Serikali kwa asilimia mia moja, umenunuliwa zaidi ya miaka mitatu/minne iliyopita, leo mkandarasi anauendesha kwa kulipwa four percent kwa mwaka. Mikataba mingi kwenye mtambo huu bado inatia mashaka Serikali kukusanya mapato yake. Sasa Mheshimiwa Waziri ndiyo nakwambia Kiti kikikamata mshahara wako usilalamike. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi napata taabu, unapoona mtambo wa TTMS ambao umenunuliwa na Serikali unaendeshwa na mkandarasi for all this time, why? Hivi hatuna local staff? Kwenye mkataba hakukuwa na package ya ku-train Watanzania wakauendesha mtambo huu? Na TCRA wameonyesha udhaifu mkubwa sana wa kuweza kuingia kwenye Network Operating Centre za operators. Na kwa vile hawaingii kwenye NOC za ma-operator hawawezi wakakamata line zote na miamala yote ya simu inayopita kwenye mtambo huu. Hamuoni haya Mheshimiwa Waziri tunasema haya miaka mitano?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna teknolojia mpya kila siku zinazaliwa, sasa imekuja IOT (Internet On things), nafikiri unaijua. Ni makampuni machache sana wanajua na wanafanya na wame-introduce software hii kwenye soko. Software hii wapewe TTCL ili waweze kushirikiana na maeneo ya kukusanya kodi kama vile TRA, waingie kwenye mitambo kwenye operating centres za makampuni ya simu. Sababu IOT ni mtandao maalum ambao mashine hizi zinazungumza wenyewe kwa wenyewe bila binadamu kuingia ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mashine hii ita- sense kuna transaction inafanyika hapa itabidi itume ile message ipeleke TRA. Kwa hiyo, mimi nakuomba Mheshimiwa Waziri kama mnataka mfano wa Ethiopia ambayo ndio juzi mnaambiwa wamefanikiwa, reli ile imejengwa kwa kusimamiwa na Kampuni ya simu ya Ethiopia. Leo Ethiopia inatengeneza vifaa vya Jeshi vya kisasa vyenye standard ya NATO, pesa zinatoka kampuni ya simu. Hivi tunangoja nini na leo Mheshimiwa Rais amezungumza asubuhi? Hivi kwa nini Serikali Mawaziri msimsaidie Rais ambaye ana uchungu wa mapato nchi hii? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mikataba hii ya simu bado tuna-weakness kubwa sana. Makampuni haya yamepewa ten percent deduction ambayo wana redeem kwenye gross turnover yao kwenye masuala ya matangazo. Hii lazima ipitiwe upya ipunguzwe. Makampuni ya simu haya yamepewa three percent kwenye management fee. Mheshimiwa Waziri wewe unajua mambo ya simu, management fee three percent ya turnover ya kampuni ya simu ni pesa nyingi sana, ndio maana utasikia unaambiwa sasa hivi your call is not reachable, yule mtu anayezungumza anazungumza nchi nyingine. Hela inatoka hapa analipwa mtu inakuwa recorded kwenye eneo lingine, hebu pitieni tena haya mambo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imenunua ndege, ndege nzuri, mimi ni mtaalamu wa masuala ya ndege. Ndege hizi zina STOL (Short Take off and Landing) zinaweza zikatua kwenye kiwanja cha mpira. Kwa abiria haiwezekani lakini kwenye dharura kwenye mambo muhimu zinatua na zina-take off kwenye kiwanja cha mpira kwa kuweka flats forty degrees down. Lakini zina advantage vile vile zinabeba abiria wengi, sabini na sita, nautical mile moja kwa gharama ya mafuta kwa kiti inalipa vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, management mpya, bado kuna tatizo la Serikali kuboresha baadhi ya viwanja vya ndege. Ndege hizi zina uwezo wa kuruka twenty four seven Mheshimiwa Waziri. Service ya ndege ni hourly bases, item za ndege zinakwenda kwa masaa, kama ndege hairuki kile kifaa hakitumiki. Sasa kwenye viwanja vyetu vya ndege vingi, unless uniambie mmeshafanya maana Bunge lililopita nililisema hili wakati huo I think Naibu Waziri alikuwa Tizeba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kitu kinaitwa PAPI (Precision Approach Path Indicator) ambayo inamsaidia rubani kutua. Tumenunua ndege za gharama kubwa sana ni lazima tuwe na usalama wa ndege na abiria. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MUSSA . ZUNGU: …Dakika kumi tayari? Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.