Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hii Wizara ya Miundombinu, vilevile namshukuru Mungu kwa kunipa huu muda wa kuchangia Wizara hii ya Miundombinu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa niaze kushukuru na kumpongeza Rais kwa uamuzi wa kuanzisha hii standard gauge. Nimpongeze Rais vilevile kwa ununuzi wa ndege bila kujali watu watasema nini, kuna watu wanakebehi kwamba ndege hazina maana, lakini tunavyojua kwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi zile ndege zilizonunuliwa ni manufaa ya Taifa zima pamoja na utalii wa ndani kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Waziri wa Miundombinu ambaye nimemwona kwenye tv akizunguka kila kona ya Tanzania kuangalia ujenzi wa miundombinu ya nchi hii, nakupongeza sana. Vilevile nimpongeze Naibu wake na Katibu wake ambao wote huwa nawaona kwenye vyombo vya habari wakizunguka na kuzungukia kuangalia miundombinu ya nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nipongeze pia ujenzi wa flyover zilipo Dar es Salaam kwani zitapunguza msongamano mkubwa uliopo Dar es Salaam ambao umesababisha shughuli nyingi za kimaendeleo zisiende. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa standard gauge ambao utaharakisha maendeleo ya nchi yetu kwa kubeba mizigo, abira na sasa Mwanza tutakuwa tunaenda kwa saa nane badala ya siku mbili. Kigoma tutakuwa tutakwenda kwa saa nane mpaka tisa badala ya siku mbili. Hivyo nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake na watendaji wake wakuu wakiwemo Mawaziri pamoja na Manaibu wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo, nia yangu ambayo nimeijia hapa hasa kwa Mkoa wangu wa Mbeya. Mkoa wa Mbeya kama mnavyoujua na wote Mawaziri mmeshafika pale, barabara ya kuingia katikati ya mji ni tatizo kubwa sana. Kama alivyozungumza mchangiaji aliyepita amesema kwamba mahali pa dakika kumi tunatumia saa mbili, ni kweli mtu ukifika Uyole kama ndege itaondoka baada ya saa mbili na nusu itakuacha, mahali ambapo tunaweza kutumia nusu saa tu kutoka Uyole mpaka Songwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya bypass ya Mbeya ambayo ni Uyole bypass kwenda mpaka Songwe tunaomba wananchi wa Mbeya ifanyiwe upembuzi yakinifu haraka ili iweze kujengwa kwani Mbeya ni lango kuu kabisa ambalo linatumia nchi zaidi ya nane kwa kutumia barabara hiyo. Barabara hiyo ni kwa ajili ya kwenda Zambia, Malawi, Congo, Zimbabwe wote wanapita njia hiyo lakini usumbufu ni mkubwa sana, naomba mtusaidie.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nina ombi kwa Waziri kuhusu uwanja wa ndege tumewahi kurudi zaidi ya mara mbili, kwa sababu tu uwanja hauna taa za kuongozea ndege pale chini. Gharama yake sijajua ni kiasi gani kikubwa, mwaka huu naona ni mwaka wa pili tukizungumzia suala hilo wakati huo huo Serikali ilishaahidi kwamba itatoa hela ingawa nimeona bajeti ya mwaka jana sijaona hata senti tano iliyoenda Songwe, kama ipo nitaomba kuiona. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, narudi kwenye Jimbo langu la Rungwe. Jimbo la Rungwe ni moja kati ya majimbo ambayo yanatoa chakula, viazi vingi mnavyoviona vinatoka Rungwe pamoja na ndizi zote zinatoka Rungwe, lakini Katika Wilaya ya Rungwe kuna kata tatu hazina barabara kabisa, hivi ninavyozungumza saa hizi zimekatika ukienda kata ya Swaya, kata ya Kinyala hakupitiki. Matokeo yake wakulima wa kule wanapata taabu kweli, tungeomba hizo barabara badala ya kuendelea kushughulikiwa na Halmashauri barabara ya kutoka Igogwe - Lubala - Vibaoni - Malangali mpaka Mbeya Vijijini tungeomba iwe barabara ya mkoa kwani pale pana mazao mengi, nazungumza sasa hivi hata tukiongozana na Waziri ataenda kukuta mazao yanavyoharibika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuyatoa mazao katika eneo hilo inabidi urudi umbali mrefu kilometa 40 halafu ndiyo uanze kupandisha nayo kwenda Mbeya kiasi kwamba wakulima wa eneo hilo pamoja na kwamba wanalima sana viazi, mahindi, maharage yananunuliwa kwa bei rahisi kiasi kwamba hawapati faida na gharama ya kilimo kile inakuwa ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeomba hiyo barabara uiangalie. Narudia hiyo barabara kama hujaiandika, barabara ya Igogwe kwenda Lubala - Vibaoni - Malangali ambayo inakwenda Swaya kwenda kutoka Mbeya Vijijini.

Hiyo ni barabara muhimu sana na kuna vyakula vingi sana, wakati kuna sehemu zingine watu wanakufa kwa njaa wanaumia kwa njaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna barabara ambayo imepandishwa daraja, ninawashukuru sana Waziri pamoja, Naibu Waziri na Watendaji wako kwa kuipandisha daraja kuwa ya Mkoa. Barabara ya kutoka Pakati - Njugilo - Masukuru kwenda mpaka mpakani. Ile barabara wenzetu upande wa Kyela wamefika mpaka kwenye mpaka. Ni sehemu ndogo ili uweze kwenda Kyela kutoka eneo la Matwebe inabidi uzunguke utumie saa mbili badala ya kutumia dakika 20, vyakula, matunda, mpunga hapo vinaaribika kwa sababu hakuna mtu ambaye anaweza akazunguka kwa kiasi kikubwa wakati huu wa mvua. Ikifika kipindi cha mvua pale mahali panakuwa ni kisiwa, huwezi tena kuenda, hizo Kata mbili zinakuwa zimebaki na kila tunapokwenda kwa ajili ya kampeni tatizo ni hilo hilo.

Naomba Waziri kwa vile umeipandisha hadhi hiyo barabara naomba uifanyie angalau ukarabati kwa sababu kule hata material ile moram ni nyingi sana maeneo yale ambayo ni kazi ndogo, kwa sababu daraja ni moja na sehemu korofi hazizidi tatu ambazo ukisizimamia zinaweza zikawa zinakapitika moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo mengine haya ninaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendeleza kujenga barabara ya Tukuyu kwenda mpaka Lwangwa kujenga barabara ya njia panda mpaka Matema hiyo nashukuku na tunaomba kila mwaka tuendelee kuzitafutia hela zile barabara, kwani zitafunguka, utalii ni mkubwa ukizungumza Matema ni utalii mkubwa sana na pale mnajenga bandari kwa ajili ya meli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka niishukuru na kuipongeza Wizara hii ni kwa kutengeneza na kutimiza ahadi. Ahadi ya kutengeneza meli katika Ziwa Nyasa. Zile meli tumeziona zimeshaingia majini na meli ya tatu ya abiria inakaribia kuisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwashukuru sana na kuwapongeza sana