Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MAHAMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri pamoja Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii nyeti katika uchumi wa wa nchi yetu. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajielekeza katika maeneo yafuatayo:-
Kwanza barabara ya Kinyanambo A – Isalavanu – Sadani – Madibira - mpaka Rujewa yenye urefu wa kilometa 141 ambayo imekuwa inawekwa katika Ilani ya Uchaguzi za mwaka 2000, 2005, 2010, 2015. Cha kusikitisha, hata kilometa moja haijawahi kujengwa kwa kiwango cha lami. Naomba sana Mheshimiwa Waziri anapokuja kuhitimisha bajeti hii, atupe maelezo ya kina, sababu zinazofanya barabara hii isianze kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, barabara ya kutoka Mtili – Ifwagi – Mdabalo – Ihanu – Isipii mpaka Mpanga TAZARA – Mlimba; barabara hii inaunganisha Wilaya ya Mufindi na Kilombero Mkoa wa Iringa na Morogoro. Vikao vyote muhimu katika kupandisha hadhi barabara hii vimefanyika mwaka 2013 na Mheshimiwa Rais ambaye alikuwa Waziri wakati huo anajua. Cha kusikitisha, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameandika barua mara nyingi Wizarani lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa. Ni vyema Mheshimiwa Waziri atuambie kwa nini hajatuma wataalam wake mpaka leo? Barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu hasa wakazi wa Tarafa ya Ifwagi ambako kuna misitu mikubwa na viwanda vya chai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka John Corner mpaka Mgololo ni barabara muhimu sana na fedha inayotumika kufanya matengenezo ni kubwa sana. Ni vema Serikali sasa ikaanza kutengeneza hata kilometa mbili mbili tu kila mwaka kuliko kuendelea kutenga fedha za kila mwaka kwenye matengenezo ya changarawe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa Serikali kukubali kurudisha Kituo cha Reli cha Mpanga TAZARA, lakini naomba sana, kituo hiki pamoja na kile cha Kimbwa kifanyiwe ukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Mheshimiwa Waziri atusaidie pamoja na minara iliyojengwa Ikweha na Igunzi, lakini wananchi hawapati mawasiliano katika Jimbo hili. Pili, minara iliyojengwa Mapanda na Isipii haisaidii wananchi waliopo kwenye maeneo husika kupata huduma hii muhimu ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema sasa Serikali ikanza Ujenzi wa Airport ya Nduli pamoja na barabara ya Ruaha National Park ambayo ni muhimu sana kwa utalii katika nyanda za juu kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.