Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika Wizara hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya mawasiliano katika Wilaya ya Ngorongoro imekuwa ya muda mrefu sasa na viongozi wamekuwa wanakuja kila mara na kuahidi kulishughulikia, lakini hawafanyi hivyo. Mfano, katika Kijiji cha Ngarasero, changamoto hii imekuwa ya muda mrefu sana. Tatizo la mtandao limekuwa sugu sasa na kufanya wananchi wanaoishi katika kijiji hiki kukosa mawasiliano ya redio tu. Naishauri sana Serikali ishirikiane katika kijiji hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ATCL; pamoja na mafanikio yaliyooneshwa na ATCL, inabidi Serikali iweke mikakati madhubuti ya soko ili kuifanya Kampuni ijiendeshe kibiashara na kuiletea nchi yetu mafaniko makubwa kiuchumi kupitia Sekta ya Usafiri wa Anga. Lazima Serikali iangalie ni mikakati ipi iliyotumika na nchi nyingine ambazo zimefanikiwa kujiendeleza kiuchumi kupitia huduma ya usafiri wa anga, mfano Ethiopia, Rwanda na UAE. Ni lazima kuwa na mikakati ambayo italeta ushindani baina ya makampuni mengine yaliyomo ndani ya nchi yetu ya Tanzania ikiwemo kubadili sheria ambazo zinabeba Kampuni nyingine ambazo zinafanya biashara sawa na siyo wazawa kama ilivyo ATCL. Mfano, Kampuni ya Fastjet.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna taarifa kuwa hata fedha za mtaji wa kuanzia hazijatolewa zote na hata zinazotolewa, zinatolewa kwa kuchelewa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu madeni ya ATCL, tumeona ahadi ya kuchukua madeni yaliyopatikana kwa ufisadi na uzembe ikitolewa bila kutimizwa kwa kipindi kirefu na kuifanya ATCL ianze kutumia mapato yake kulipia uzembe huu uliosababishwa na mipango mibaya ya usimamizi mbaya wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kubinafsisha ATCL kwa Shirika la Ndege la SA (Afrika Kusini), mali nyingi za ATCL zilichukuliwa na Serikali na nyingine kuuzwa. Hii inalifanya shirika sasa kutokuwa na mali zake binafsi na kusababisha kuongezeka kwa gharama za juu za uendeshaji. Naiomba Serikali isaidie kurudisha mali hizi ili kulipunguzia shirika mzigo mkubwa sana wa kiuendeshaji ukizingatia ATCL ndiyo kwanza inaanza kufanya kazi. Tatizo hili linaweza kuifanya Kampuni hii kufilisika tena na hatimaye kuwa ATCL tena kama ilivyokuwa huko nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali itueleze, mali ziko wapi hasa? Kwa nani na lini zitarudishwa ili kuweza kulisaidia shirika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naomba kuwasilisha.