Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kuwa miongoni mwa wanaochangia hoja hii kwa bajeti hii ya 2017/ 2018. Naanza kwa kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa jinsi inavyotenga fedha na kuendeleza miundombinu mbalimbali ya barabara, madaraja na mawasiliano. Pia pongezi kwa Waziri, Mheshimiwa Profesa Mbarawa kwa umakini na ufuatiliaji wa karibu sana katika miradi yote na bila ya kuchoka, yeye na wasaidizi wake hatimaye kuona kila lililopangwa linakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa Mbunge toka Mkoa wa Pwani na kuona jinsi ambavyo nachangia kuomba kujengewa barabara za lami katika wilaya zilizozopo Mkoa wa Pwani, ikiwemo barabara ya Kisarawe – Vikumburu – Mlandizi – Maneromango. Hii imekuwa adha kubwa sana kwa wananchi wa huko hasa nyakati za mvua. Awamu zote katika ilani yetu imekuwa ikiahidi lakini hadi leo haijafika kokote. Naomba sana, barabara hii ipatiwe fungu la kutosha na kuweza kujenga. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, pia naomba ahadi za Marais wetu zitimizwe, kwani barabara ya Nyamwage – Utete - Mkuranga – Kisiju – Bungu – Nyamisati, hizi barabara ni muhimu sana kwa wananchi wa maeneo hayo na hata kwa wasafiri wengine na kukuza biashara na kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa ujenzi wa reli (standard gauge) ambayo Mkoa wa Pwani tutasaidiwa kwa maana mbili; ajira, usafiri na uuzaji wa vyakula na hiyo itainua kipato cha wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mkiwa maeneo hayo ya ujenzi, kipaumbele cha ajira kianze kwa wananchi walioko jirani na ujenzi wa hiyo reli.