Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa utendaji mzuri, yeye na Naibu Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara na Watendaji Waandamizi wa Wizara. Kazi inayofanywa na Wizara inaonekana na inaheshimiwa kwa umma wa Watanzania. Hongera sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimboni kwangu nina barabara mbili za Kitosi - Wampembe yenye urefu wa kilometa 68 na ile ya Nkana – Kala yenye urefu wa kilometa 67. Barabara hizi zote mbili za Mkoa wa Rukwa, kupitia Bodi ya Barabara na RCC tuliomba zipandishwe hadhi na Kamati ya Kitaifa ilikuja na kuridhia. Aliyekuja ni Katibu Mkuu wa sasa wa TAMISEMI (Mussa Iyombe), lakini hazijapandishwa licha ya Serikali kupandisha hadhi barabara nyingi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba zipandishwe hasa ya Kitosi na Wampembe. Mheshimiwa Rais alitoa ahadi kusaidia barabara hizi na wakati alipokuwa Waziri, aliweza pia kutoa fedha shilingi milioni 500 kwa barabara ya Kitosi na Wampembe kuboresha matengenezo. Nashangaa hamjaipatia fedha ya kutosha na inaenda mipakani. Naomba iongezewe fedha, sh. 84,000,000/= hazitoshi. Inaweza kusababisha barabara kufunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Kata ya Kala ipate mawasiliano ya simu. Ni Kata iliyoko mpakani mwa Ziwa Tanganyika. Nimefanya ufuatiliaji mkubwa bila mafanikio. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri atanisaidia Kala iwe na mawasiliano?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari Kata ya Ninde, Wampembe na Kala ziko kando ya Ziwa Tanganyika, hazina bandari hata moja. Kuna umuhimu mkubwa kupata Bandari Wampembe na pia kujenga Gati Ninde na Kala ili wananchi waweze kupata huduma ya usafiri wa meli kwa usalama. Kwa hiyo, nawasilisha maombi Serikalini kuwa bandari ijengwe Wampembe na gati zijengwe Ninde na Kala. Ahsante.