Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa barabara ya kutoka Mlowo (Mbezi) kwenda Kamsamba (Momba) kuelekea Kilyamatundu (Kwela) hadi Kasansa na hatimaye Kibaoni (Katavi). Ni vyema Serikali itengeneze barabara hii kwa kiwango cha lami. Mosi, hii barabara inaunganisha Mikoa mitatu ya Songwe, Rukwa na Katavi na kwa kuwa ni Sera ya Serikali kutengeneza kwa kiwango cha lami barabara zinazounganisha mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wananchi wanaoishi maeneo yanayopitiwa na njia hii wanalima mazao ya kahawa, mpunga, mahindi, ufuta, alizeti, mtama, maharage na mazao mengineyo. Naishauri Serikali itengeneze barabara hii kwa kiwango cha lami ili wananchi waweze kusafirisha mazao yao kupeleka sokoni kirahisi. Soko kuu la mazao katika ukanda huu linapatikana Mlowo – Mbozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na barabara hiyo hapo juu, pia kuna barabara ya kutoka Mji Mdogo wa Mlowo, Wilaya ya Mbozi kupitia Vijiji vya Shiwinga – Isansa - Magamba na kuelekea Kata ya Magamba, Wilaya ya Songwe. Hii barabara ni ya muhimu kwa sababu inaunganisha Halmashauri ya Mbozi na Songwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mazao mbalimbali kama vile kahawa, mahindi, maharage, alizeti, ufuta na mengineyo yatasafirishwa kirahisi. Pia makaa ya mawe yanayochimbwa Kijiji cha Magamba yatasafirishwa kirahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.