Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Naipongeza Serikali katika ukamilishaji wa daraja la Mto Kilombero. Hakika daraja hili ni ukombozi mkubwa sana kwa wakazi wa Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliahidi kujenga na kumaliza barabara ya Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa Mpepo – Londo –Namtumbo (TI6) katika kiwango cha lami. Naiomba Serikali kutekeleza ahadi hii ya ujenzi wa kiwango cha lami kwa kuwa kuwa barabara hii inahudumia maeneo muhimu ya uzalishaji wa mazao ya nafaka (mpunga). Ni eneo ambalo Taifa linategemea chakula (mpunga). Hivyo kuwepo kwa barabara ya lami itaongeza tija sana kwa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii, aidha itakuwa ni njia ya mkato, hivyo kuokoa muda na fedha kwa wakazi wa Mikoa ya Ruvuma na Njombe kuja Dar es Salaam na Dodoma (HQ). Wakati mchakato wa ujenzi wa barabara ya lami (TI6) unaendelea, naiomba Serikali kutoa kipaumbele na kuongeza bajeti ya ukarabati ya maeneo korofi, kwani fedha iliyotengwa haitoshi kabisa. Ni kipande cha kilomita 25 tu za changarawe, zimetengwa kwa urefu wa barabara yenye urefu zaidi ya kilomita 300.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado Wilaya ya Malinyi ina changamoto ya mawasiliano ya simu katika Kata za Ngoheranga, Kilosa Mpepo, Biro na Sofi. Aidha, minara iliyotengwa na TiGO kupitia ruzuku ya UCAF haifanyi kazi kwa kiwango cha kuridhisha na baadhi ya minara hiyo haifanyi kazi kabisa kutokana na hitilafu/upungufu wa kiufundi. Ahsante.