Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nawapongeza Wataalamu wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya na TANROAD kwa ufanisi mzuri wa kazi wanayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie upande wa marine. Hii Taasisi ni kubwa, inazo meli 15 ambazo zinatakiwa zifanye kazi katika maziwa yetu matatu kwa maana ya Ziwa Nyasa, Tanganyika na Victoria. Hizi meli zinaweza zikafanya kazi katika maeneo haya na kupata mapato makubwa ya kuongeza kuwa GDP. Itasaidia kuongeza ufanisi wa maeneo mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika lina madeni ya wazabuni karibu shilingi bilioni saba. Pamoja na hayo, wafanyakazi nao hawajalipwa zaidi ya miezi 11. Hii inasababisha kukatisha tamaa watumishi wa Shirika hilo. Ikumbukwe hawa watumishi wanategemewa na familia zao. Fedha iliyotengwa mwaka 2016 kwenye bajeti ya shilingi bilioni 1.4 haijatoka hata moja. Hii inasababisha watumishi kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.

Pamoja na kuwa wanadai, wafanyakazi wamekuwa na moyo wa kizalendo wa kufufua meli moja inayoenda Ukerewe ambayo imeweza kusaidia wananchi kwa huduma hiyo.

Mheshimiwa Spika, Watumishi hao hawajalipia Bima za Afya tangu mwaka 2014. Wafanyakazi hawapati huduma za afya pamoja na michango ya Mashirika ya Umma; NSSF na PPF.

Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango gani na Shirika hili kubwa lililo na meli 15 ambazo fedha nyingi zimetumika lakini hazifanyi kazi? Kwenye bajeti iliyoisha Serikali ilitenga Bajeti ya shilingi bilioni 50 nayo haijapata hatma za fedha hizo zimefanya kazi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kwa kutenga fedha kilomita 49.7 toka Bariadi kwenda Maswa. Tunashukuru sana kwa kazi hiyo nzuri. Naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi hiyo nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri mnayofanya kwa kufufua mashirika haya ya Serikali yanayoweza kuifanya nchi kuwa na mapato mengi. Mfano, TRL, ATCL, TTCL na TPA. Marine mkiitunza hakika nchi hii itakuwa inapata mapato mengi. Tunayo meli ya MV Umoja ina uwezo mkubwa wa kubeba behewa zaidi ya 20 kupeleka Uganda moja kwa moja.