Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika nchi nzima na ambayo tayari imekwisha kufanyika. Mawaziri hawa ni mahiri, wasikivu na wachapakazi sana. Hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mengi yaliyofanywa na yanayoendelea kufanywa na Wizara hii, naomba nishauri yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyombo vya Usafiri kwa Watu Wenye Ulemavu (Mabasi). Ipo haja kwa Serikali kuliangalia hili kwa kuwaagiza wamiliki wa Public Transport kuhakikisha vyombo vyao vinazingatia mahitaji maalum. Hili litawezekana endapo kutakuwa na Sheria ya kuwabana wamiliki hawa wakati wa usajili; kuwa chombo hakitasajiliwa kwa huduma za kijamii kama kitakuwa hakijakidhi vigezo ama kama kitakuwa hakina miundombinu ya kuwezesha mtu mwenye ulemavu hasa wa viungo kupanda pasipo shida yoyote ama pasipo kubebwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ndege. Kwa ndege ndogo (kati ya abiria 5 – 25) zinazofanya safari zake ndani ya nchi yetu miundombinu yake si rafiki kwa watu wenye ulemavu kwani upana wa ngazi zake ni mdogo sana na hakuna Ambulift. Ushauri wangu ni; Unguja wana ngazi pana (Uwanja wa Unguja) ngazi hii ni ya mbao, inatumika pale inapotokea mtu hawezi kupanda kwa kutumia ngazi za ndege husika (yaani zile ndege ndogo hasa coastal na kadhalika)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu kumpakia kwenye ndege si sahihi kabisa, hivyo naomba sana Serikali yangu sikivu ihakikishe uwepo wa Ambulift na hizi ngazi za mbao kwenye viwanja vya ndege kote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwepo wa Ambulift, lift na hizi ngazi za mbao kwa ndege ndogo zitasaidia wagonjwa, wazee na watu wenye ulemavu kutobebwa wakati wa kupanda ndege kitu ambacho ni hatari kwa anayebebwa na anayebeba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.