Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi yake nzuri. Mheshimiwa Waziri, kama atakumbuka miezi miwili iliyopita alipata nafasi ya kutembelea Uwanja wa Musoma ambapo aliahidi kuujenga kwa kiwango cha lami. Nashukuru kwamba ametenga fedha kwa kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja inawasumbua watu wa Musoma kwa sababu wataalam walikuja kuangalia maeneo ya kupanua uwanja huo, wakavuka barabara upande wa pili wakasema hapo patafanyiwa tathmini. Napenda kufahamu ni kweli uwanja huo utavuka barabara kuelekea upande wa magharibi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, kuna kitega uchumi chetu cha mwalo wa kupokelea samaki Mwigobero. Mwalo huu ulichukuliwa na bandari na tuliomba turudishiwe; tulimweleza Mheshimiwa Waziri na akatukubalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa tunasubiri bado hatujapata jibu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri. Nategemea majibu mazuri.