Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Abdallah Haji Ali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kiwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ABDALLAH HAJI ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu muweza wa mambo yote duniani. Pili, nampongeza Mheshimiwa Spika kwa kusimamia majukumu yake vyema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia angalau machache kati ya mengi kwa Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Kwa nia njema kabisa Serikali katika kutafuta changamoto ya usafiri ilileta meli ya kisasa ili kupunguza tatizo la usafiri kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo. Lengo kuu la ujio wa meli ile ni kupunguza tatizo la usafiri kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo, lakini cha kushangaza meli ile haionekani ikifanya huduma iliyokusudiwa na tatizo lile la usafiri bado lipo vilevile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wazi kwamba malengo na nia njema iliyokusudiwa haikufikiwa, lakini kubwa ni kwamba meli ile Wizara husika na Serikali kwa ujumla wanafahamu ilipo na matumizi yake. Hivyo ni vyema wananchi wakapata maelezo sahihi ili wafahamu meli ile iko wapi na inatumika vipi? Naomba Mheshimiwa Waziri atoe maelezo japo kidogo juu ya kutokufikiwa kwa dhamira nzuri iliyokusudiwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala zima la viwanja vya ndege. Kumekuwa na malalamiko makubwa kwamba viwanja vingi havina taa hivyo ndege zetu zinashindwa kutua usiku. Katika ulimwengu huu wa sasa wa sayansi na teknojia safari ni wakati wowote iwe usiku au mchana ili kwenda na wakati na kurahisisha mambo yawe sawa. Naishauri Serikali kuliona suala hili na kuwapatia huduma walipa kodi wa nchi hii ili waweze kwenda na wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuweka taa katika viwanja vyetu vya ndege ni miongoni mwa kuboresha miundombinu ili iwe mizuri na kuwaweka watu wetu katika hali ya kisasa zaidi.