Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

kiti, TTCL ni moja ya mashirika yaliyo chini ya Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Taasisi hii ya TTCL ni kampuni Kongwa, kuliko kampuni zote za mawasiliano Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni jambo la kusikitisha kwamba TTCL imekuwa nyuma sana katika masuala ya kiteknolojia kiasi kwamba imekuja na wateja wachache sana ikilinganishwa na kampuni nyingine za simu. Napenda kutumia fursa hii kuishauri Serikali yangu kuongeza nguvu ya uwekezaji katika Kampuni hii kama ilivyofanya kwa ATCL kwa kununua ndege ili kusaidia kui-boost ATCL. Ni wakati sasa wa kuiboresha TTCL na sina mashaka na nia nzuri ya Mheshimiwa Rais kwani tayari mmeshamteua kijana mahiri kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na changamoto kubwa hasa katika suala zima la kuongeza nguvu ya ringtones na mimi binafsi nimekuwa nikijiuliza, je, Serikali inanufaika kiasi gani na ringtones hizi? Kwa kuwa zimekuwa zikiingizwa kwenye simu zetu bila hata idhini zetu. Kwa mtazamo wa haraka, ni hakika Kampuni za Simu zinapata fedha za kutosha kutokana na huduma hii. Mashaka yangu makubwa yapo kwenye malipo kwa vijana wenzangu na wasanii wote kwa ujumla pale nyimbo zao zinapotumika kama ringtones.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kuishauri Serikali yangu kuanza kulifuatilia suala hili kwa ukaribu kwa kuhakikisha Kampuni za Simu zinalipa mapato yanayotokana na ringtones kwa Serikali na wasanii ambao nyimbo zao zinatumika wanapata stahili zao kwa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango huu, naomba kuunga mkono hoja.