Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaipongeza sana Wizara hii kwa kazi nzuri inayoendelea. Ilani ya CCM inaelekeza vizuri kuwa barabara zilizounganisha wilaya na mikoa zitajengwa kwa lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anaijua hii barabara ya Iringa – Kilolo – Dabaga – Idete. Mheshimiwa Waziri alifika Kilolo anaijua; ipo kama kilometa 27, lakini barabara hii kilometa tano ni za Jimbo la Iringa na kilometa 15 ni Jimbo la Kalenga na kilometa saba ni Kilolo. Hizi zote kwa pamoja ndiyo unapata barabara ya Iringa – Kilolo – Dabaga – Idete. Barabara hii ina mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa, ndiko ambako mbao nyingi zinatoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila nilipouliza swali kuhusu barabara hii jibu linakuwa la kutia matumaini lakini utekelezaji wake hakuna. Naomba sana barabara hii itengewe fedha ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Barabara ambayo inatakiwa ipandishwe daraja ni Dabaga
- Ng’ang’ange, Bomalang’ombe – Mwatasi – Mufindi. Vikao vyote vilipitisha ombi la barabara hii. Hivyo tunaomba barabara hii ipande daraja iwe ya mkoa.