Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara nyingi zilizopo katika Jimbo la Vwawa zimekuwa hazipitiki kipindi cha masika. Tunaomba Serikali kupitia Mfuko wa Barabara kuzifanyia matengenezo ya mara kwa mara. Kuna barabara ya kilometa 10 alizoahidi Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni. Pia ili Mkoa mpya wa Songwe uunganishwe vizuri ni vyema Serikali ikajenga barabara zifuatazo kwa kiwango cha lami:-
(a) Barabara ya Njiapanda ya Iyula – Idiwili – Itezya hadi leje.
(b) Barabara ya Vwawa – Nyimbili – Hezya hadi Ileje.
(c) Barabara ya Viwawa - Igamba Magamba hadi Mkwajuni Songwe.
(d) Barabara ya Ihanda – Chindi hadi Chitete – Momba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuimarisha reli ya TAZARA ili iweze kutoa mchango mkubwa wa uchumi katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Hali ya Shirika hili si nzuri kabisa na wakati huo huo barabara nyingi zimekuwa zinaharibika sana kutokana na mizigo mikubwa. Ili kuimarisha kilimo, madini, ufugaji ni vizuri reli hii ikahudumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa majengo ya ofisi na nyumba za watumishi katika Mkoa wa Songwe. Nini hasa mpango wa Serikali katika kujenga nyumba na majengo ya ofisi katika mkoa huo mpya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, utoaji wa huduma wa Wakala wa Umeme na Ufundi uimarishwe ili kutoa huduma nzuri za utengenezaji wa magari ya Serikali na umeme kwenye majengo ya Serikali. Hivi sasa gharama ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la TTCL na TCRA yaimarishwe ili yaweze kutoa mchango mkubwa katika utoaji huduma na kuchangia kukuza mapato ya nchi yetu. Ni vyema Serikali ikayasaidia zaidi.