Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. AIDA J. KHENAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mawasiliano ya Simu. Kulingana na umuhimu wa mawasiliano kwa binadamu ili kuweza kutimiza malengo yao kwa wakati ni vema Serikali ikamaliza tatizo kwa kupeleka minara ya simu kwenye maeneo ambayo bado hayajapata mawasiliano. Kwa mfano Jimbo la Nkasi Kusini, Wilaya ya Nkasi iliyopo Mkoa wa Rukwa, Kata ya Kala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Meli ya MV Liemba. Meli hii imekuwa ya muda mrefu na imechoka, Serikali kwa nini isituletee meli mpya ili kuokoa maisha ya wananchi wa Ziwa Tanganyika? Suala la barabara inayotoka Sumbawanga – Kanazi limechukua muda mrefu na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wanaotoka Namanyere, Kilando, Kabwe na maeneo mengine ya Wilaya ya Nkasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Kiwanja cha Ndege cha Manispaa ya Sumbawanga. Mpaka sasa wananchi wa Sumbawanga wanashindwa kuendelea na shughuli zao wakisubiri kulipwa baada ya tathmini. Nashauri Serikali baada ya tathmini, iwalipe wananchi hawa na kama kuna matatizo ya kifedha basi waruhusiwe kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Usalama katika Bandari; kuna kila sababu ya Serikali kufanya tathmini ya kutosha katika maeneo ya bandari, kwa sababu kumekuwa na changamoto na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na wafanyakazi wa bandari. Suala la fedha kutofika kwa wakati, nalo linakera, ni tatizo kwenye maeneo mengi nchini na kupelekea usumbufu mkubwa kwa kutomaliza miradi mbalimbali ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Barabara Kujengwa Chini ya Kiwango; suala hili limekuwa endelevu katika mikoa yetu. Nashauri Serikali iwachukulie hatua wakandarasi wote wanaofanya kazi chini ya kiwango na kutoa taarifa kwenye maeneo mengine ili wawafahamu wakandarasi wazuri na wabaya ili wasirudie kuwapa kazi wakandarasi wasio na sifa.