Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. LOLESIA J.M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Serikali na Wizara ya ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa kazi nzuri inayofanyika katika Taifa letu hasa katika ujenzi wa barabara na reli. Katika hotuba nimeona jinsi ambavyo Serikali imepanga kuanza rasmi ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Geita – Bukoli
– Kahama. Napongeza kwa mpango huo mzuri kwani utaongeza na kuimarisha uchumi kwa Mikoa ya Geita na Shinyanga. Vile vile nashukuru kwa kilomita moja ya lami kwa barabara ya Geita – Bukombe. Pamoja na shukrani hizo ningependa kupata ufafanuzi, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kilomita 10 za lami katika mamlaka ya Mji mdogo wa Katoro/Buserere itaanza kutekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni upandishwaji hadhi wa barabara ya Katoro – Kamena – Mwingiro. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kipindi kirefu sasa tumeomba barabara ya Katoro – Kamena – Mwingiro, ipandishwe hadhi kuwa barabara ya Mkoa. Mapendekezo hayo yamepitishwa katika ngazi zote kuanzia kwenye Baraza la Madiwani pamoja na DCC. Nilipoangalia kwenye bajeti ya 2017/2018 sijaona hatua yoyote ya Wizara katika utekelezaji wa ombi. Hivyo, napenda kujua ni lini sasa barabara ya Katoro – Kamena – Mwingiro itapandishwa hadhi kuwa barabara ya Mkoa? Barabara hii ni kiunganishi muhimu sana kati ya Wilaya ya Geita na Wilaya ya Nyang’hwale na kwa msingi huo ikiboreshwa (ikipandishwa hadhi) itasaidia sana kuimarisha uchumi ndani ya Mkoa wa Geita. Kwa sababu hiyo, nashauri Serikali kupitia Wizara ilichukue ombi letu na kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja.