Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo yangu yote ya Ofisini kwa Naibu Waziri na Katibu Mkuu yazingatiwe.
(i) Kukasimu barabara ya Mugeta – Misingo – Mekomariro (Bunda) hadi Sirorisimba (Butiama) na Serengeti.
(ii) Kutangaza mkandarasi wa barabara ya Nyamuswa – Bunda (ahadi ya Mheshimiwa Waziri 31/12/2016) aliposimama Kata ya Nyamuswa na kuahidi kutangaza mkandarasi ifikapo Februari, 2017.
(iii) Kutangaza mkandarasi kipande cha Sanzate hadi Nata. Nasikitika kuona kipande hiki kimerukwa badala yake Wizara ilitangaza barabara ya Nata. Kwangu naona kama sikutendewa haki na hasa ikizingatiwa hii Lot ilitakiwa kwisha kabla ya kutangaza huku. Naomba haki itendeke.
(iv) Uwanja wa Ndege Musoma, Mheshimiwa Waziri alishasema anatafuta shilingi bilioni 10 za ukarabati wa uwanja huu mapema 2016/2017. Nasikitika kuona bajeti iliyotengwa ni shilingi bilioni tatu badala ya shilingi bilioni 10. Naomba suala hili lizingatiwe.
(v) Reli ya Arusha – Musoma. Reli hii toka mwaka 1975 inapewa ahadi hadi leo. Tunaomba kwa miaka mitano watu wa Musoma waone jitihada ya Serikali katika kujenga reli hii.
(vi) Bandari ya Musoma ilikuwa ikipokea meli ya MV Victoria, MV Butiama na MV Umoja. Nimeona juhudi za Wizara za kutengeneza meli hizo, tunaomba meli hizo zikitengenezwa zifike Musoma. Matengenezo ya Bandari ni kidogo sana.