Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, nimpongeze Waziri na watendaji wa Wizara kwa kazi inayofanyika sasa. Pongezi hizo zinatokana na ukweli kuona Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameonesha njia na uongozi mahiri wenye kulenga kuibadili Tanzania na kupiga hatua za haraka katika maendeleo. Yapo mambo mengi yamefanyika ikiwemo ujenzi wa reli ya standard gauge, kufufua ATC, kutenga asilimia 40 ya mapato na kuelekeza katika shughuli/miradi ya maendeleo. Pamoja na pongezi hizo, yapo maeneo muhimu ya kuchangia kama ifuatavyo:-
(i) Daraja la Sibiti linalojengwa sasa na shilingi 3.5 bilioni zimetengwa lakini barabara hiyo yenye daraja linalounganisha Mkoa wa Simiyu na Singida lakini katika bajeti hiyo ni lini upembuzi yakinifu utafanyika?
(ii) Wilaya ya Mkalama ni mpya na haina hata kilomita moja ya lami na zipo shughuli nyingi za kiuchumi, tunaomba Wizara itenge fedha za ujenzi wa kilomita 30 za lami kutoka Iguguno –Ndugahi yalipo Makao Makuu ya Wilaya.
(iii) Bado wananchi wa Mkalama wanapata shida ya mawasiliano kutokana na kutokuwepo minara ya kutosha. Tunaomba Wizara iweke mikakati ya kuhamasisha makampuni ya simu kuweka minara hasa katika Kata za Kinyampanda, Mwangeza, Ibaga, Mpambala, Msingi na Kinyangiri.
(iv) Zipo barabara ambazo hazihudumiwi na TANROAD wala Halmashauri pamoja na kuwa maeneo husika yana wakazi wengi pia ni maeneo yenye uzalishaji mkubwa mazao hasa mahindi na alizeti. Hivyo, naomba Wizara ichukue jukumu hili kwa kufungua barabara husika ya Msingi – Yulansoni – Lyelembo -Kitumbili (kilomita 25).
(v) Ipo barabara ambayo inaunganisha mikoa miwili kupitia Wilaya ya Mholame nayo tunaomba itengewe fedha, upembuzi yakinifu ufanyike. Ni barabara ya Haydom - Kidasafa – Nkungi - Ilongero - Singida (kilomita 93.4).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.