Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ni kigezo kimojawapo cha kuongeza uchumi au kudhoofisha uchumi kwa ujumla katika Tanzania yetu. Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa ambayo imeendelea kudumaa kiuchumi na moja ya sababu ni kukosa barabara zenye uhakika na kusuasua kwa kuchelewa kujenga barabara na kutengewa fedha ndogo zinazochelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mpanda - Koga yenye urefu wa kilomita 1.0 na Mpanda - Uvinza zimesubiriwa na wananchi kwa muda mrefu waondokane na kero hii ya kulala barabarani kunakosababishwa na barabara mbovu na madaraja kukatika. Nini hatua ya dharura inachukuliwa kuwakomboa wananchi ili waondoke katika kero hii? Kuchelewa kwa bidhaa katika maeneo ya biashara, mazao kuoza yakiwa njiani, je, Serikali haioni kwamba kupitia barabara hizi mbovu zinaendelea kuwafanya wananchi hawa wa Katavi kuendelea kuwa maskini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii iliyopangwa kwa mikoa hii inayoungana mitatu Tabora-Kigoma na Katavi, tulitegemea itengwe bajeti ya kueleweka ili imalize hizi barabara. Mfano barabara ya Kibaoni - Mpanda ikamilike kwa wakati lakini mpaka sasa haijulikani nini kinasababisha barabara hizi zisikamilike kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zilizotengwa kufanyiwa marekebisho ya changarawe na udongo, Wizara ingeangalia maeneo ambayo hayapitiki kabisa yarekebishwe yote. Kwa jiografia ya Mkoa wa Katavi hakuna barabara za kuchepuka hivyo daraja linapovunjika/bomoka basi watu hawasafiri wala kuendelea na safari. Serikali hii sasa iwe na vipaumbele kutokana na mahitaji ya wananchi wake na wasifanye wanachotaka wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba changamoto hizi zifanyiwe kazi mapema:-
(i) Barabara zinazojengwa katika Manispaa ya Mpanda hazina viwango na hazina mitaro. Ni barabara mpya lakini zina viraka, je, ni kigezo gani kinatumika kila wakati kuendelea kuwapa kandarasi wakandarasi hawa?
(ii) Kucheleweshwa pesa kwa kandarasi hii inaleta shida na miradi kuchukua muda mrefu imekuwa ni kero sasa.
(iii) Usafiri wa reli Mpanda - Tabora – Dodoma, Serikali ihakikishe ujenzi wa reli ya kisasa sio siasa tu bali iingie katika utekelezaji.