Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ZUBEDA H. SAKURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha mchango wangu katika Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia za ujenzi wa barabara; ili kupitisha ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami hasa barabara ya Tunduru – Mangaka - Matemanga, wananchi na wakazi wa vijiji vilivyopo kwenye Tarafa ya Nakapanya, baadhi ya wakazi hawajalipwa fidia mpaka sasa licha ya kukidhi vigezo vya kulipwa fidia zao. Vilevile wahanga wa Vijiji vya Songambele, Namakambale, Nakapanya, Pacha ya Mindu, Mtonya, Misufini, Namiungo, Mnazi mmoja na Majimaji nao wanadai fidia zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na malalamiko mengi juu ya utoaji wa fidia kwa wahanga, bado wakazi wa Vijiji vya Muhuwesi, Chingulungulu, Msagula, Sevuyanke, Temeke, Sisi kwa Sisi, Mkapunda, Ngalinje, Mchangani, Kalonga, Lambai na Tunduru Mjini nao wanadai fidia kutokana na ujenzi wa barabara. Je Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wakazi wa maeneo hayo wanalipwa fidia kwa wakati?

Mheshimiwa Mwenyekiti, upanuzi wa uwanja wa ndege Dodoma; pamoja na mahitaji makubwa ya upanuzi wa uwanja wa ndege Dodoma, bado haitoleta tija katika mipango miji na usalama wa wakazi wa maeneo ya karibu kutokana na uwanja huu kuwa karibu sana na makazi ya watu. Mpaka sasa, bado wananchi wanaendelea kubomolewa nyumba na wengine bado kulipwa fidia wakati uwanja wa ndege wa Msalato ndiyo uliostahili kupewa kipaumbele na kuleta tija kwa matumizi sahihi ya viwanja vya ndege. Je, Serikali imetumia vigezo gani na kuzingatia nini katika ujenzi wa kiwanja hiki karibu na makazi ya watu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano; kuna changamoto kubwa ya mawasiliano hasa ya redio na simu katika Kata ya Nalasi Wilayani Tunduru. Upatikanaji wa taarifa umekuwa ni changamoto kubwa na kusababisha wananchi kukosa mawasiliano na taarifa. Je, ni lini Serikali itaboresha huduma ya mawasiliano hasa masafa ya redio?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ubovu wa barabara; akiwa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya Serikali kujenga barabara kwa kiwango cha lami kuunganisha Wilaya ya Mbinga hadi Mbamba Bay Mkoani Ruvuma, Wilaya ya Nyasa yenye kilometa 67, wakati Rais wa Awamu ya Nne akizindua madaraja pacha ya Ruhetei A, B na C. Hali halisi ya barabara ya Mbinga hadi Mbamba Bay sasa ni mbaya, hasa ukizingatia ni kipindi cha masika. Barabara hii haipitiki na wananchi wanakwama sana. Pamoja na Serikali kila mara kueleza kuwa Serikali ipo katika hatua za mwisho za kupata Mkandarasi, ahadi hii ya barabara inaendelea kuchukua muda kutekelezwa na kusababisha hasara kubwa za kiuchumi na kijamii. Je, Serikali inatoa kauli gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.