Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza utendaji kazi mzuri kwa Viongozi na Watendaji wote wa Wizara na Taasisi zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TTCL, iimarishwe zaidi kwa vitendea kazi vya kisasa ili iweze kufanikisha malengo yake kwa kufikia kutoa huduma za mawasiliano katika maeneo na vijiji vyote ndani ya Tanzania kwa ufanisi mkubwa. Mitandao ya simu ya Tigo, Airtel, Vodacom haina nguvu katika baadhi ya maeneo na maeneo mengine mawasiliano hakuna kabisa huko Zanzibar, hivyo waongeze nguvu ili wateja wapate huduma katika sehemu zote huko Zanzibar mfano, Chukwani, Mji Mkongwe na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi za Serikali na Taasisi zake watumie huduma za simu za TTCL pia wahimizwe kulipa madeni kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Posta, liongeze nguvu na kujipanga zaidi katika huduma ya kusafirisha pesa na kupokea fedha kwa njia ya haraka ili watu wavutike kutumia huduma yao badala ya kutumia mawakala wengine wa kupokea na kupeleka fedha nchi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Nawatakieni kazi njema na nguvu katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.