Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana kwa kazi nzuri za kuwahudumia wananchi na kwa ushirikiano mnaonipa kuwahudumia wananchi wa Karagwe. Naomba nichangie yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru barabara ya Nyakahanga-Nyabiyenza-Nyakakika imekasimishwa TANROADS na kutengewa shilingi milioni 150 kwa mwaka wa fedha 2017/2018, pamoja na shukrani nawaomba tena nipo chini ya miguu yenu barabara hii mniwekee nguvu
ipande officially kwenda TANROADS. Bahati nzuri wote wawili mmeshatembelea Karagwe na nimewalilia sana kwa kuonesha umuhimu wa hii barabara kwenye kukuza uchumi wa Wilaya na nchi yetu kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inahudumia kambi za JWTZ, barabara hii inatuunganisha na nchi ya Rwanda. Mheshimiwa Rais aliahidi kilometa tano za lami, nimeshakaa na Madiwani na kupitia Baraza la Madiwani tumeridhia kwamba kilometa hizi za lami ziende kwenye barabara tajwa Nyakahanga-Nyabiyenza-Nyakakika eneo korofi sana la Kajura Nkeito. Nawaomba sana fedha hizi zitengwe na kuletwa ili tuweze kudhibiti eneo hili korofi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji kivuko Single Custom ili kuimarisha biashara kati ya Wilaya ya Karagwe na nchi ya Rwanda kwenye eneo la Chamhuzi Kata ya Bweranyange ambalo lipo kwenye barabara tajwa kwenye aya ya kwanza na ya pili hapo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara nyingine nawapongeza na kuwashukuru kwa ushirikiano mnaonipa kuwahudumia wananchi wa Wilaya ya Karagwe. Nitashukuru iwapo nitapata reaction yenu wakati wa majumuisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, thanks and God bless.