Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hoja zifuatazo katika Wizara hii kuhusu Jimbo la Sikonge:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande cha barabara kutoka Mibono hadi Kipili kwenye barabara ya Sikonge – Mibono – Kipili hakijatobolewa kwa muda mrefu, wakati inaunganisha Sikonge Makao Makuu ya Wilaya na Kata mbili za Kipili na Kilumbi ambako kuna zaidi ya wakazi 45,000. Kuna uchumi mkubwa sana, maelezo aliyonipa Naibu Waziri kuwa eti kutobolewa kwa barabara hiyo kunahitaji fedha nyingi sana sh. 12,000,000,000, sasa hoja yangu nauliza ni lini Serikalini sh. 12,000,000,000 zikawa nyingi? Au kwa sababu mzigo mzito mpe Mnyamwezi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua ingekuwa maeneo mengine ya nchi ingekuwa imeshatengenezwa japo kwa kiwango cha udongo/changarawe. Naomba Serikali ijipange ili barabara hiyo itobolewe ifike hadi Kipili kama siyo mwaka huu basi mwaka ujao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande cha barabara kutoka Ipole hadi Lungwa ni cha muhimu sana kama kweli tunataka kuunganisha Mikoa ya Mbeya na Tabora. Lini kipande hicho kitajengwa kwa kiwango cha lami? Ndugu yangu Mheshimiwa Waziri namwambia kuwa Mbunge wa Sikonge ni mzigo mzito sana kulingana na jiografia yake na alijionea mwenyewe, mbona sijaona majibu yake kwenye hotuba yake?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano; nimeshaongea sana na Dkt. Sasabo ambaye ni Katibu Mkuu – Mawasiliano kuhusu kukosekana kabisa kwa mawasiliano ya simu katika Kata za Nyahua, Igigwa, Kiloleni na Ngoywa na pia mawasiliano hafifu kabisa kwenye Kata za Kipili, Kilumbi, Kiloli, Kitunda, Mole na Ipole. Fedha za mawasiliano vijijini zinatumika lakini Sikonge tuna njaa sana ya mawasiliano. Naomba sasa kwa maandishi haya Wizara hii itutendee haki na sisi tupate mawasiliano ya uhakika kama ilivyo kwa maeneo mengine ya nchi, watu wanatumia simu lakini hawana mawasiliano ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja, lakini kwa masharti ya kusikilizwa kilio cha wananchi wa Sikonge.