Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na wataalam wao kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao. Nipongeze Serikali kwa kuanza kujenga reli kwa kiwango cha SGR, pia nimpongeze Waziri kwa kazi ya ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mtwara. Naomba Serikali kuona umuhimu wa kukarabati uwanja wa ndege wa Mtwara kwani umechakaa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kuiomba Serikali kuhusu kuharakisha na kuongeza kiwango cha pesa kwa barabara ya Mtwara, Newala, Masasi kwa mujibu wa mkataba. Serikali pia ianze ujenzi wa reli ya Mtwara - Mchuchuma na Liganga Mbamba bay. Reli hii ni muhimu sana kwa uendeshaji wa bandari ya Mtwara.