Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sina budi kumshukuru Mwenyenzi Mungu, kwa kunijalia afya njema na leo hii kuweza kusimama kwa ajili ya kuchangia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipatia nafasi hii. Nampongeza Katibu Mkuu wa Chama changu CUF Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na uongozi wa Taifa kwa kazi kubwa aliyonayo kupambana na wanafiki walioko ndani ya chama chetu, kututaka kutugawa na kusambaratisha chama chetu. Nasema chama chetu kiko imara Maalim Seif chapa kazi tuko pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu uzazi salama. Takwimu za hivi karibuni zinaonesha wanawake 30 wanafariki kila siku kwa kujifungua. Hii ni idadi tu ya wale wanawake wanaofika kwenye vituo vya afya na wanaofika hospitali kwani wengi wanajifungulia majumbani, idadi ni kubwa na hii hali inatisha. Wanawake wengi tunapoteza maisha kwa uzazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo changamoto nyingi zinazo msababisha mwanamke kufariki. Kwanza ni kukosa vifaa tiba na dawa; pili, lishe bora na umaskini unachangia pamoja vituo vya afya kujengwa mbali na wananchi, hivyo, inapelekea kupata matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naishauri Serikali bajeti ya Wizara ya Afya iongezwe na wale watu wanaofanyakazi kwenye sekta ya afya waboreshewe pia maslahi yao ili wapate kufanyakazi kwa weledi mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza Serikali kwa kudhibiti na kupambana na madawa ya kulevya katika nchi hii vijijini na mijini. Waathirika wengi wanaopoteza nguvukazi ni vijana walio chini ya umri wa miaka 18. Watoto hawa wanatoroka shule na baadaye wanajiingiza katika vitendo vya kutumia dawa za kulevya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dawa za kulevya zinachangia kiasi kikubwa maambukizi ya UKIMWI na magonjwa ya akili, naishauri Serikali kupitia sober house ni lazima akiingia mle walipie ada, wengi wao hawana uwezo, wazazi wao tayari wameshawatelekeza, kwa hiyo Serikali iwatibu bure kupitia Wizara ya Afya kwa sababu hawana uwezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu ukatili wa kijinsia. Wanawake wengi katika nchi hii wananyanyasika, wananyanyaswa na waume zao, kupigwa hata kuuawa, kwa sababu ya mapenzi tu. Wengine ni waume zao, wengine ni wapenzi tu, hilo jambo lipo, mashuleni, vyuo vikuu watoto wanajiingiza kwenye mapenzi na baadaye wanauawa. Hili jambo ni la kutiliwa nguvu sana kwa sababu linapoteza vijana wetu wengi kwa ukatili.