Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima na uhai. Kabla sijaanza naomba niunge mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wanaifanya. Kwa kweli Serikali ya Awamu ya Tano ikiongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli imefanya mambo mengi na makubwa katika nyanja mbalimbali. Kila eneo kwa kweli imefanya kazi kubwa na ni kazi ambayo kwa kipindi kifupi imeweza kuonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi za pekee vilevile zimfikie Mheshimiwa Mama Samia Suluhu, Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Kassim Majaliwa ambaye yeye ndiye Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni. Shukrani nyingine za pekee ziwafikie Waheshimiwa Mawaziri wote ambao wako kwenye Serikali hii ya Awamu ya Tano, hongereni sana kwa kazi nzuri na kubwa ambazo mnazifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nataka nizungumzie maeneo makubwa mawili; kwanza nizungumzie afya ya mama na mtoto pamoja na eneo la UKIMWI kwa ujumla wake. Kabla sijaenda kwenye maeneo hayo, niseme kwamba Serikali hii ina dhamira ya makusudi kabisa ya kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanaishi kwa kuwa na afya bora na nzuri zaidi na ndiyo maana kwa misingi hiyo hata ukiiangalia bajeti ya mwaka 2016/2017 inatofautiana sana na bajeti ya mwaka 2017/2018. Hii ni kuuthibitishia umma kwamba Rais, Mheshimiwa Magufuli ana dhamira ya dhati kuwaweka Watanzania kwenye afya nzuri na afya bora zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nizungumzie afya ya mama na mtoto. Takwimu zinaonesha kwamba katika vizazi hai 100,000 wanawake 556 hufariki dunia. Wanawake hawa 556 ambao wanafariki dunia hii takwimu ni kubwa zaidi. Hatutaki mwanamke hata mmoja afariki wakati analeta kiumbe kingine. Kwa kweli kwa misingi hiyo hili jambo ni lazima litazamwe kwa jicho la pekee kabisa ndani ya Wizara hii. Nasema haya kwa sababu kubwa za msingi. Sababu ya kwanza, takwimu hizi kwa mara ya mwisho zilikuwa 446 hivi lakini sasa zimetoka kwenye 446 zimefika kwenye 556, hapa ni lazima tupaangalie kwa namna ya pekee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiachana na vizazi hai, tunaingia kwenye eneo la watoto, watoto 25 kati ya 1,000 wanapoteza maisha. Watoto hawa wanaopoteza maisha lengo letu ndiyo waje kuwa watu wazima hatimaye washike mamlaka ndani ya Taifa lao. Sasa kama hivi leo tunawapoteza watoto hawa nini matokeo ya baadaye? Hili jambo ni lazima liwe kwa mapana yake kama ambavyo tumeangalia katika maeneo mengine tusiruhusu mtoto afe wakati akija duniani. Naiomba Serikali/Wizara ihakikishe kwamba wanaboresha maeneo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine, akina mama waliambiwa waende na vifungashio hospitalini. Leo hii akina mama wanabeba vifungashio vyao na akina mama hawa ni maskini, tunafanyaje juu ya jambo hili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, narudia tena kuunga mkono hoja.