Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri sana wanayoifanya ya kuongoza Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunatambua kama alivyoeleza kaka yangu Mheshimiwa Lwakatare, tetemeko lililotukumba Mkoa wa Kagera, napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Waziri alipofika pale Jimboni kwangu Misenyi kuna eneo moja linaitwa Kabyaile akakuta zahanati imeenda chini yote kwa sababu ya tetemeko, akanipigia simu akaniuliza Mheshimiwa Kamala hapa zahanati yako imekwenda bado unahitaji zahanati au unahitaji kituo cha afya. Nikamwambia Mheshimiwa mimi ni nani kuombwa na Waziri nipewe kituo cha afya nikaendelea kung’ang’ania jambo dogo! Nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa sababu kituo cha afya hicho kimejengwa na kinafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua ziko changamoto zinaendelea, lakini nichukue nafasi hii kumshukuru Waziri wa Nishati na Madini kwa kuhakikisha umeme unafika pale kama alivyoahidi Mheshimiwa Rais, umeme umefika pia nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais alituahidi kutupa access road ya lami ya kwenda pale Kabyaire na lami hiyo sasa itajengwa kwenda pale Kabyaire ili wagonjwa waweze kufika pale bila matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kwa kuwa tunayo na ahadi ya Makamu wa Rais ya kuhakikisha tunapata barabara nzuri ya kwenda Mgana basi tuunganishe hii access road ya Kabyaire na access road ya kwenda Hospitali Teule ya Mgana ili mambo yaweze kwenda vizuri.

Pia nichukue nafasi hii kushukuru kwa kweli kwa mambo yote hayo ambayo yamefanyika ndani ya kipindi kifupi na wenzetu wa Bukoba Vijijini walipoona Kabyaire sasa inapata kituo cha afya na wao wakatuomba wakasema tunaomba nasi tupate huduma kutoka kwenye kituo hicho na hatuna sababu ya kuwabagua wenzetu, niombe basi Serikali ifanye utaratibu iunganishe barabaa ya Kabyaire pamoja na ile inayokwenda Bukoba Vijijini kwa kaka yangu Mheshimiwa Rweikiza ili wananchi wote waweze kupata huduma safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa siyo mkweli kama nitamaliza kuzungumza hapa bila kueleza ukweli kwamba Hospitali Teule ya Mgana (DDH) pamoja na taarifa nzuri zilizopo ya fedha tunazooneshwa kwamba tumepokea kwa ajili ya kutoa huduma, lakini ukweli pale huduma ya mama na mtoto hakuna, hakuna huduma ya bure kama inavyotarajiwa itolewe, hili limekuwa tatizo kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Baraza la Madiwani walikuwa na kikao na wakazungumza, Mwenyekiti wa Halmashauri akaniambia wanakaa na mimi nikamwambia nilishamueleza Mwenyekiti wangu wa Halmashauri wakiona jambo lolote wakae na wakiona hawaoni siendi wajue bado naamini wanafanya kazi.

Kwa hiyo, wamekaa na wamezungumza walipomaliza akanipigia akasema Mheshimiwa mambo hayaendi, nikasema sasa kama mambo hayaendi, basi kabla mimi mwenyewe sijaja nitamuomba kwanza Mheshimiwa Waziri wa Afya kwa sababu leo atawasilisha hoja yake basi nitamuomba atusaidie na yeye kuja hapo Mgana aweze kuangalia na kujifunza nini kimetokea, Hospitali ya Mgana ambayo ilikuwa inatoa huduma nzuri kwa watoto sasa haitoi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kumuomba Mheshimiwa Waziri aungane nami tuende tutembelee hiyo hospitali ya Mgana tuweze kuondoa hii pandora’s box inayojitokeza ya maajabu ambayo yameanza kujitokeza ya hospitali kushindwa kutoa huduma….

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.