Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana. Kama ulivyonitaja mimi naitwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki. Kwanza kabisa naomba nitoe shukrani za dhati kabisa kwa wananchi wa Wilaya Maswa na hasa Jimbo la Maswa Mashariki, kwa kuikomboa Wilaya yetu kutoka Upinzani wa Majimbo mawili, Maswa Mashariki na Magharibi. Wametupa kura nyingi, mimi na mwenzangu wa upande wa Magharibi, tumemuondoa Shibuda na Kasulumbayi aliyekuwa anajiita Yesu kwa kura nyingi ambazo hata kwenda Mahakamani walikata tamaa. Tumeshinda vizuri kwa kishindo na napenda kusema kwamba hata kura za Magufuli, Mheshimiwa Rais wetu, tumempa kura nyingi sana Wilaya yetu ya Maswa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kuungana na wenzangu wengi walivyoongea kuunga mkono hotuba nzuri kabisa ya Mheshimiwa Rais, aliyoitoa tarehe 20 Novemba, hotuba hii ilikuwa imesheheni maudhui ambayo Watanzania walipenda wayasikie. Kero zilizokuwepo, ambazo zilikuwa ni wimbo kwa wenzetu wa upinzani, ndani ya hotuba ya tarehe 20 Novemba ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli ilitoa majibu kwa kero zote zilizokuwa zinatukabili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hotuba hii ukiitazama kwa undani, ilikuwa imegawanyika katika sehemu kubwa mbili, lakini katikati kuna kiungo.
Sehemu ya kwanza ya hotuba hii ilikuwa ni matumizi makubwa, kwa maana ya ahadi zilizotolewa na Mheshimiwa Rais na ahadi zilizomo ndani ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo tumeitumia kuinadi kwa wananchi na wakatuamini wakatupa Kura nyingi. Ahadi ni nyingi ambazo zimegusa matatizo ya wananchi wa Tanzania. Ukitizama kwa upande huo, kweli kabisa kuna matumizi makubwa ambayo yanahitaji pesa nyingi kuhakikisha ahadi hizi zinakamilika na wananchi wanapata yale mabayo tuliwaahidi. Katika hotuba hii ya Meshimiwa Rais John Pombe Magufuli, upande wa pili wa hotuba unaonyesha ni jinsi gani tutapata pesa hizo, ni mikakati gani iliyopo, Serikali inaunda mikakati ipi kuhakikisha pesa zile zinapatikana na pesa zikipatikana basi ahadi hizi ziweze kukamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katikati ya mapato na matumizi kuna barriers ambazo zinafanya matumizi haya yasiweze kukamilika iwapo majipu aliyoyasema Mheshimiwa Rais yataendelea kuwepo. Majipu haya ndicho chanzo au kikwazo cha mapato makubwa ya nchi yetu. Jipu la kwanza alisema rushwa, jipu la pili alizungumzia mfumo mbovu, jipu la tatu akazungumza sheria mbovu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ukubali, katika mwili wa binadamu kweli anaweza akapata majipu, kwa tukisema majipu tunazungumzia mwili wa binadamu, kuna majipu mazuri, yamekaa sehemu nzuri, mtu anaweza kavaa shati mwingine asione, lakini kuna majipu mengine yamekaa sehemu mbaya. Na kuna majipu mengine yamekaa usoni, lakini majipu mabaya ndiyo yanayoharibu hata mwenendo wa binadamu kutembea, badala ya kutembea kawaida unatembea kama bata. Mojawapo ni hili jipu la Sheria ya Ununuzi. Ukienda katika Halmashauri nyingi kuna magari hayatembei, bado mazima eti kwa sababu ya Sheria ya Ununuzi. Kipuri hakinunuliwi kwa sababu ya Sheria ya Ununuzi. Tunashukuru Mheshimiwa Rais alisema hili litakuja Bungeni, Wabunge tumsaidie na mimi ninapenda kusema kwamba Wabunge tuwe tayari kwa kumsaidia Mheshimiwa Rais kutengua sheria hii na kuirekebisha kwa manufaa ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hicho ni kiungo. Tukianza na matumizi, kuna matumizi makubwa, kuna ahadi kubwa, hizi lazima zitekelezwe na hakuna mjadala. Issue hapa ni kutafuta pesa, Serikali itumie mbinu kuweza kuhakikisha kwamba tunapata pesa, tunakusanya pesa za kutosha ili tuweze kukamilisha ahadi hizo. Sasa pesa itapatikana vipi? Ndipo tunarudi kule kule kusema kwamba kama tumeamua kuwekeza kwenye viwanda, tumeamua kuwekeza kwenye kilimo ni lazima tutengeneze miundombinu, miundombinu ambayo itakuwa ni friendly ku-invest kwenye kilimo, friendly ku-invest kwenye viwanda. Tuwe na miundombinu ambayo itafanya uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazotumika kila siku. Bidhaa kama toothpick, tissue paper, napkins, bidhaa ndogo ndogo ambazo kila siku zinatumika, tuna-import kutoka nchi za nje, basi iundwe miundombinu kuhakikisha kwamba na sisi tunaweza kufanya production kwa cheap cost ili tuweze kuingia kwenye competition ambayo itamfanya mwananchi wa kawaida aweze kununua bidhaa zetu, aache kununua bidhaa za nje.
Kwa mfano, ukitazama General Tyre. General Tyre kumbe ilizimwa tu, ilizimwa kwa sababu production cost ya General Tyre ilikuwa ni kubwa. Uki-produce tairi moja la General Tyre gharama yake ni sawa sawa na tairi nne za kutoka Malaysia. Wana-produce kwa cost ndogo, malighafi wanazo za kutosha, ile production in technology ni simple inafanya tairi inakuwa produced kwa low cost, matokeo yake inatoka nje kwenye market inakuwa competitive kwa sababu wananchi watanunua kwa bei nafuu. Lakini kwa sasa hivi technology ya General Tyre, ukifyatua tairi moja tairi lile linakuja kuuzwa laki nne halafu muuzaji ambaye ni mjasiriamali anayeuza matairi ana tairi lingine la kutoka Malaysia linauzwa shilingi 80,000/=. Lazima mwananchi atanunua tairi ya Malaysia ataacha tairi ya General Tyre.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali ya John Pombe Magufuli, kwa kushirikiana na Mawaziri wake, Mheshimiwa Muhongo tupelekee umeme, tutengeneze barabara hata kama ni kwa kukopa, tupelekeeni maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisiendelee kuongea hayo, lakini naomba niongelee kuhusu Maswa. Maswa ni Wilaya kongwe, Wilaya ya siku nyingi. Tumeomba siku nyingi tupandishiwe hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji kutoka Halmashauri ya Mji Mdogo, haijapandishwa. Tunaomba tupandishiwe Halmashauri ya Maswa iwe Halmashauri ya Mji. Kuna faida ya Halmashauri kuwa ya Mji, tunaomba Halmashauri ya Mji wa Maswa. Tunaomba kilometa tatu za ahadi ya Mheshimiwa Rais alizoahidi Maswa, Waziri mhusika tunaomba Maswa mtupe kilometa tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Victoria lipo karibu na sisi, leo nimesikia majibu ya Mheshimiwa Waziri hapa, eti tunahitaji pesa katika mradi wa kutoa maji kutoka Ziwa Victoria, tunahitaji zaidi ya bilioni 730 na zaidi, ambazo ni sawa sawa na Euro milioni 331. Pesa zinazotafutwa ni za wafadhili. Sijaona sehemu Serikali inasema ina mkakati wowote wa kutafuta pesa hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri mchakato wa kuleta maji Maswa ufanyike haraka iwezekanavyo. Mtuletee maji katika Wilaya zetu zote za Mkoa wa Simiyu, na wewe ni shahidi unatoka Mkoa wa Simiyu, hatuna maji Mkoa ule, tunaomba mtuletee mitambo ya maji haraka iwezekanavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuchukua nafasi hii, kwa sababu tunakwenda kwenye viwanda, Mkoa wa Simiyu unazalisha mazao yanayotokana na mifugo. Tunaomba wawekezaji waje, kuna ngozi tunauza, ngozi ya ng‟ombe inatupwa kwenye mnada ng‟ombe wakishachinjwa ngozi inatupwa, inauzwa shilingi 1,000 au shilingi 800 wakati ngozi moja ya ng‟ombe inatoa mikanda ya kiuno 50. Mkanda mmoja wa kiuno tunanunua shilingi 50,000 madukani, ng‟ombe mmoja anatoa mikanda 50, ni sawa sawa na shilingi milioni moja, lakini ngozi ile inatupwa kwenye minada yetu na ikiuzwa inauzwa shilingi 800/=, it is a shame. Ngozi ya mbuzi inauzwa shilingi 200/=. Sisi tukichinja mbuzi Mkoa wa Simiyu ngozi ya mbuzi tunatupa kule haina thamani yoyote. Tunaomba mtuletee viwanda vidogo, wawekezaji karibuni Maswa. Zaidi ya hapo naunga mkono hoja, ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)