Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOS NYIMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru Waziri Mheshimiwa Ummy Mwalimu pamoja na Naibu wake Waziri Dkt. Kigwangalla, kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wanaifanya ndani ya Wizara hii. Pia nimpongeze Rais wangu aliyetokana na Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri na kubwa anayoifanya katika Taifa hili la Tanzania. Wananchi wa Tanzania tuna furaha kwa kazi kubwa ambayo anaifanya na kuwatendea haki Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ni kubwa, Dada yangu Ummy Wizara ni kubwa, kazi na majukumu uliyokuwa nayo ni makubwa, lakini haina budi ukiwa kama mwanamke mwenzangu nikupongeze kwa ufanisi mkubwa wa kazi na uwezo uliokuwa nao wa kazi, kuweza kumudu Wizara hii kubwa na Wizara ambayo imebeba watu wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikizungumza watu wote, majigambo ya Wabunge, majigambo ya Makatibu Wakuu, majigambo ya waendesha boda boda yote yanategemea afya zao na umezibeba wewe dada yetu Ummy pamoja na kaka Kigwangalla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisiache pia kuzungumza suala zima la afya kwa watoto. Mheshimiwa Waziri umelizungumza katika kitabu chako, umelizungumza na kuliongea kwa kina suala zima la afya ya watoto katika ukurasa wa tano, umelizungumza na umelitendea haki, ila dada yangu nikuombe ukiwa kama mwanamke kumbuka unapokwenda labour unapofikwa na uchungu. Unayoyafanya yote ni mazuri lakini wajibu wetu kukukumbusha kuna baadhi ya maeneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatupaswi kulaumu, tunapaswa kukuambia ili ukumbuke na kuangalia maeneo mengine. Unapokwenda labour mwanamke unaujua uchungu na dada yangu Ummy una watoto uchungu unauelewa. Watoto wamefikwa na janga kubwa linalowasumbua sasa la kubakwa, hatuna budi kama mwanamke angalia kwa jinsi ya pekee tatizo hili tunalitatuaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninalizungumza Dada Ummy huwezi kulitatua peke yako, lazima kuna baadhi ya watu mshirikiane au Wizara mshirikiane. Lazima ushirikiane na Wizara ya Mambo ya Ndani, lazima ushirikiane na Wizara ya Katiba na Sheria. Dada Ummy ni nafasi yako kama mwanamke kaa nazo Wizara hizi muone tatizo hili mnalitatuaje. Leo kilio cha kila mwanamke ndani ya Nchi hii, ubakaji wa watoto na unyanyasaji wa watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna njia nyingi za unyanyasaji wa watoto, lakini kwa sasa yenye sura ya pekee ndani ya Tanzania ni suala la ubakaji. Nimeambiwa jana Dada yangu Faida amesimama mpaka amefikia kulia, suala la ubakaji ni suala kubwa, Dada Ummy unafanya kazi kubwa lakini kaa na Wizara zingine hutalitatua peke yako na kulimaliza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninalizungumza hivi kwa sababu, Wizara hizi imefika wakati unapokwenda Mahakamani unaambiwa limekwama Wizara ya Mambo ya Ndani kwa maana polisi, lakini polisi ukifika ukifuatilia unaambiwa limekwama hatuna maelezo ya kutosha ndani ya Wizara ya Afya. Tulione suala hili linakwendaje na suala hili Dada Ummy linahitaji pia elimu ya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wenzetu wengine hawafahamu kwamba mtoto unapompeleka ukamtia maji, tayari baadhi ya uthibitisho unaufuta kabisa. Inapaswa lazima kama mwanamke usimame na kutoa elimu ya kutosha ili tuone tatizo hili kama Serikali na kama viongozi tukiwa tuna nia moja na lengo moja ya kulitatua tatizo hili limalizike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa wa 26, ulizungumza kwa makini na kwa kuitolea maelezo ya kutosha hospitali ya Muhimbili. Ndani ya mwezi mmoja uliokwisha nilikuwepo Muhimbili kwa muda wa siku tatu, ilinibidi nikae pale. Panapostahili sifa binadamu apewe sifa. Mmefanya kazi kubwa lakini naamini kazi hii anayewatia nguvu na kukuwezesheni ni Mheshimiwa Rais. Inapofika wakati kama viongozi tusiwe wingi wa kulaumu tukakosa kushukuru. Unapoizungumzia hospitali ya Muhimbili uwe umekwenda umefika. Kuna tofauti kubwa ya nyuma tulipotoka na sasa hivi, lakini kwa sababu kuna baadhi ya watu nilipoenda, nilifanya kazi nikiwaona nisiache kuwataja kwa majina, lazima niwasifie. Kiongozi unapopata muda, posho tunayowalipa haitoshi kwa madaktari lakini basi...(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALOS NYIMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kuunga mkono hoja, ingawa nimeambiwa nina dakika kumi.