Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika hotuba ya Waziri wa Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu dakika ni chache kwanza kabisa mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, hongera sana Dada yangu Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu pamoja na Naibu Waziri Kigwangalla kwa kazi nzuri mnayoifanya, nina uhakika kabisa tunapoelekea vifo vya wanawake na watoto, lakini pia matatizo pamoja na ukatili wa kijinsia utapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa dakika ni tano, naomba nijikite katika suala moja ambalo limezungumzwa hapo jana kwa kirefu na aliweza kulizungumza Mheshimiwa Faida, na mimi pia naomba nijikite katika suala hilo. Suala la ukatili kwa watoto ni kubwa, kwa kiasi kikubwa sana na ukatili huu dhidi ya watoto katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri pia imeelezwa katika ukurasa wa 55.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite na kwa kutoa mifano katika suala hili. Utafiti uliofanywa na Jumuiya ya Maimamu kule Zanzibar unaonyesha kwa kiasi kikubwa ukatili dhidi ya watoto, watoto wamekuwa wakilawitiwa, watoto wamekuwa wakinajisiwa kwa kiasi kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti uliofanywa mwaka 2014/2015 umebainisha kuwa suala hili ni janga. Watoto wameharibiwa kwa kiasi kikubwa, watoto wa miaka kuanzia minne na kuendelea. Kwa mujibu wa utafiti huu uliofanywa, unaonesha kwamba nchi za Magharibi kwa kiasi kikubwa zimetumia mbinu mbalimbali kuhakikisha kwamba nchi za Afrika zinaidhinisha mapenzi ya jinsia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya mila, tamaduni na desturi zetu imekuwa ni vigumu. Kwa maana hiyo, ipo nguvu kutoka nje ambayo kwa mujibu wa utafiti huu inawatumia baadhi ya walimu wa madrasa kule Zanzibar, lakini pia walimu wa shule za msingi inawatumia. Walimu hawa wanapewa pesa na kuhakikisha kwamba wanawalawiti watoto ili kuandaa kizazi ambacho itakuwa ni rahisi baadaye kuwa na kizazi cha watoto ambao wanashiriki mapenzi ya jinsia moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti huu nipo tayari kuuthibitishia Bunge hili na kukutanisha na wale ambao tayari wamekwisha fanya utafiti huu na kubaini ni kwa jinsi gani watoto wetu wameharibiwa na watoto wengine wameshakuwa wazoefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa utafiti huu Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar alishakabidhiwa ripoti, pia katika Siku ya Wanawake Duniani pia walizungumzia hawa maimamu kuonesha ni kwa jinsi gani wazazi, walezi, lakini pia walimu wa madrasa ambao ndio tunawategemea kuwalea na kuwakuza watoto wetu katika maadili ndio wanaoshiriki, lakini pia walimu wa shule za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe tu angalizo kwamba sisi kama wazazi, hata wageni wanaokuja nyumbani kwetu tusijenge tamaduni za kuhakikisha kwamba wanalala na watoto wetu kwa sababu ndiyo hao wanaowaharibu watoto wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifuatilia kwa undani zaidi ukazungumza na watu ambao wanashiriki mapenzi ya jinsia moja, atakuambia mjomba ndiye aliyeanzisha tatizo hilo, mwingine atakuambia ni ndugu wa baba ndiye aliyeanzisha tatizo hilo. Kwa hiyo, tujenge tamaduni watoto wetu tusiwaweke karibu na ndugu wanaofika katika familia zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili tatizo ni kubwa na ni janga, ni janga la kitaifa. Tunaandaa kizazi ambacho baadaye kitakuwa ni tatizo kubwa katika nchi yetu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono.