Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MWANTUMU D. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali yangu chini ya Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufulikwa jinsi anavyoisimamia Serikali yake, nasema ahsante. Pia nimshukuru Waziri, Mheshimiwa Ummy na Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla kwa kusimamia vyema Wizara yao kikamilifu, nawapongeza sana, Mwenyezi Mungu awasaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu huduma ya afya ya uzazi na watoto. Vifo vitokanavyo na uzazi bado vinaendelea japokuwa vimepungua lakini wajawazito wengine hawana elimu kutokana na umbali kutoka wanakoishi mpaka kwenye vituo vya afya. Kwa hiyo, naishauri Serikali wapatiwe huduma elekezi, japo wauguzi wa vituo mbalimbali wasogee vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini wajawazito wengi wanapata operesheni, kwa nini iwe hivi? Watoto wengi sasa wanaozaliwa afya zao zinakuwa si nzuri. Aidha, wamekuwa wadogo sana au wamelegea. Mzazi anahangaika mpaka anachoka. Huduma wodini madaktari wanajitahidi sana, lakini wodi ndogo hazina ukarabati, vitanda vidogo, inafikia hatua kitanda kimoja wazazi watatu au wawili, hivi na magonjwa kila mtu na yake ukizingatia maambukizi ni mengi. Kwa hiyo, naishauri Serikali ifanye juhudi zake ili ipanue wodi au ukarabati kwenye hospitali zetu zilizokuwa zimechakaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.