Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu mpendwa kwa yote yaliyotekelezwa ndani ya kipindi hiki cha mwaka mmoja kupitia Wizara hii. Pili niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa utendaji wenu mahiri na jinsi mnavyojituma kulitumikia Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee Mental Health Act 2008 sheria namba 28. Sheria hii ipo toka mwaka 2008 lakini mpaka leo ni miaka tisa kanuni hazijatungwa ama kuandaliwa. Kutokuwepo kwa kanuni kumesababisha sheria hii kutoanza kutumika na hivyo kupelekea wagonjwa wa akili na walemavu wa akili kukosa haki zao za msingi. Naomba kufahamu, ni lini kanuni hizi zitaandaliwa na Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana? Pia kuna upungufu wa madakatari (kuna madaktari 15 tu nchi nzima).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee msamaha wa matibabu kwa wenye ulemavu. Wakati linajibiwa swali langu Bungeni, Serikali ilikiri kutokuwa na utaratibu wa kuwabaini watu wenye ulemavu wenye vipato duni hivyo kupelekea Watanzania kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali ikubali kuwaingiza watu wenye ulemavu ambao wana vipato duni kwenye huu msamaha wa matibabu. Kwanza iwabaini kwa kuwapatia vitambulisho ili wanapofika hospitali pasiwe na usumbufu kwao. Nafahamu kuna mpango wa Serikali wa kuwapatia Watanzania wote bima ya afya. Naipongeza Serikali kwa mpango huu. Mpango huu ni long term, hivyo ninaiomba Serikali wakati tunasubiri ione ni jinsi gani itawaangalia watu wenye ulemavu kwa masuala mazima ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee watoto wenye vichwa vikubwa. Kadi Toto Afya haiwakubali watoto wenye vichwa vikubwa, wanaambiwa wao ni wagonjwa, kadi hii kwa nini inawabagua watoto hawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee upungufu wa dawa za walemavu wa akili. Ninaiomba Serikali iongeze bajeti ama itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya ununuzi wa dawa za akili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu watu wenye ualbino, limekuwa ni ombi la muda mrefu kuwa sunscreen lotion zinunuliwe ama ziagizwe na Serikali kama dawa zingine zinavyoagizwa ama kununuliwa. Ninaiomba Serikali yangu sikivu ilizingatie ombi kwani mafuta haya ni muhimu na ni kama chakula kwa wenzetu wenye ualbino.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna uhitaji mkubwa wa vifaa vya ku-detect kansa kwa hatua za awali (Kliogan).Vifaa hivi vitakuwa msaada mkubwa si tu kwa watu wenye ualbino bali kwa Watanzania wote maana kansa imekuwa tishio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaipongeza Serikali kwa zoezi la ugawaji wa vifaa mbalimbali kwenye hospitali zetu vikiwemo vitanda. Katika vitanda hivi, je Serikali ilizingatia ombi letu la vitanda vya kujifungulia wanawake wenye ulemavu? Kama haikuzingatia kwa kweli wanawake wenye ulemavu tuna uhitaji mkubwa wa vitanda hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye hospitali zetu kuna uhitaji mkubwa wa wakalimali wa lugha ya alama kwa wagonjwa ambao ni viziwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kodi kwenye taulo za kike (pads), ninaiomba Serikali iondoe kodi kwenye taulo hizi kutokana na umuhimu wake na kulinganisha na vipato vya wanawake wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na ninaomba ufafanuzi wa hoja zangu wakati mtoa hoja anamalizia.