Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ANGELINA S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha niwapongeze sana kwa kazi nzuri mnayoifanya katika Wizara hii kwa kushirikiana na Naibu Waziri na timu nzima ya wataalam. Mwenyezi Mungu aendelee kuwabariki muendelee kuwatumikia Watanzania. Vilevile nichukue fursa hii kutoa shukrani kwa mara nyingine kwa mgao wa gari la wagonjwa, hakika mlitusaidia kwa kiasi kikubwa sana kusaidia huduma ya mama na mtoto katika jimbo langu hususan Kituo cha Afya Sangabuya ambako gari lilipelekwa na Kituo cha Afya Karume linakotumika pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni kwamba Manispaa ya Ilemela haina Hospitali ya Wilaya mpaka sasa, kwa juhudi za Halmashauri na kwa msaada wa Serikali Kuu jengo la wagonjwa wa nje tayari limepanuliwa. Tunaomba Wizara isaidie ukamilishaji wa hospitali hiyo ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando na Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Manispaa ina vituo vya afya vitatu tu kati ya 19 vinavyotakiwa. Pamoja na mapungufu hayo, vituo tulivyonavyo bado vina mapungufu mengi sana. Naomba Wizara yako katika majengo ya theatre yatakayojengwa nchini walau kituo kimoja kipate, hasa kituo cha Buzuruga ambacho kina mapungufu mengi. Kwa kuainisha Kituo cha Afya Buzuruga, kinahudumia wagonjwa takribani 25,877 lakini hakina jengo la upasuaji, wodi ya wanaume wala wodi ya akina mama waliojifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Karume kinahudumia wagonjwa 25,654 lakini hakuna nyumba za watumishi pamoja na jengo la wagonjwa wa nje. Kituo cha Afya cha Sangabuye hakina nyumba za watumishi, hakuna wodi ya watoto, hakuna wodi ya wanaume. Tunaomba walau tupate jengo la wodi kwa wanaume na watoto.

MheshimiwaMwenyekiti, tuna upungufu mkubwa wa watumishi katika kada ya wateknolojia maabara, wateknolojia dawa, wahudumu wa afya pamoja na watunza kumbukumbu za afya.