Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wataalam wa maabara kwenye vituo vya afya iwe kipaumbele. Kwa Biharamulo DMO anatoa pesa mfukoni mwake kulipa watu watatu wenye vyeti vya taaluma ya maabara ambao wanafanya kazi kwa kujitolea. Watu hawa hawalipwi mshahara, wanalipwa posho na DMO kutoka kwenye mshahara wake. Naomba waingizwe kwenye ajira na wabakizwe pale pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa CHF kwa wajawazito wa Wilaya ya Biharamulo, tutafikiwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, PLHIV na walemavu wajumuishwe kwenye asilimia kumi ya Halmashauri inayokwenda kwa vijana na wanawake. Haya ni makundi maalum zaidi, wakipata pesa hizi zitawasaidia kufanya shughuli za kiuchumi na hivyo kuweza kulipia CHF.