Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapa hongera sana kwa kazi nzuri sana wanayoifanya chini ya usimamizi wa Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa ujumla. Mheshimiwa Waziri Ummy naomba kukumbushia vitanda vitano na magodoro yake, ahadi uliyoniahidi na mimi nikaenda kutoa ahadi ya vitanda vitano, magodoro na mashuka yake katika Kituo cha Afya cha Malya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi hiyo imekuwa ya siku nyingi, naonekana muongo kwa sababu ya kutotekeleza ahadi iliyopitia kwangu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri. Mimi naheshimika kwa kutosema uongo kwa wananchi wangu ambao nawaamini na wao wananiamini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri naomba utekelezwaji wa ahadi hiyo ya vitanda vitano katika Kituo cha Afya cha Malya, Jimbo la Sumve. Nawatakia kila la kheri katika utekelezaji wa majukumu yaliyo mbele yenu.