Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mweyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuongeza watendaji kazi wa maendeleo ya jamii ili kutoa ushauri kwa jamii kuacha tabia za wanandoa kutengana na kusababisha malezi ya watoto kuwa shida, hali inayosababisha kuwepo watoto wengi wa mtaani. Tatizo la watoto hawa linapelekea kuwepo kwa watoto wanaozaa kabla ya wakati jambo ambalo linaendelea kuzalisha watoto wa mtaani. Nashauri Serikali ili kupunguza ongezeko la kasi la watu wanaolitegemea taifa moja kwa moja liongeze watoa elimu kwa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuzungumzia juu ya uhaba wa dawa za kutibu na kuzuia magonjwa nyemelezi ya watu walioathirika na UKIMWI ambayo yanasabisha vifo vingi. Nishauri hospitali kugawa dawa za kufubaa na ziambatane na dawa za magonjwa nyemelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kushauri kwamba vitendea kazi viongezwe katika hospitali, katika maeneo mengine hawana vifaa vya kuhifadhia watoto njiti. Niishauri Serikali kuweka zahanati kila kata ili kurahisisha ufikaji wa wagonjwa kwenye huduma. Pia niishauri Serikali kuhakikisha inaongeza dawa ya kuwezesha kupima UKIMWI kwani mara nyingi zimekuwa adimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba matengenezo katika Chuo cha Maendeleo Kibaha na Shirika la Elimu FDC ili kuweza kutekeleza malengo ya kuanzishwa kwake. Majengo yamechakaa sana na hakuna majiko, wanapika kwenye majiko yaliyochakaa na finyu, pia yanahatarisha afya za wapishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali kukiangalia kwani kilikuwa kinatoa wahitimu ambao wanasaidia sana kuleta mabadiliko kwa jamii. Niombe mortuary ya Kibaha iongezwe kwani ajali zote zinapotokea Morogoro majeruhi na maiti huletwa Tumbi Kibaha pia tuongezewe na dawa.