Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namkupongeza sana Waziri kwa hotuba yake nzuri yenye ufafanuzi wa mambo mbalimbali ya sekta ya afya. Pili, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Pamoja na kuunga mkono hoja hii, naomba kuchangia mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa vituo vya afya ni muhimu sana hasa katika maeneo ya vijijini ambako wananchi wengi wapo, vituo vya afya lazima viwe na wataalam wa kutosha na viwe na daktari msaidizi, wauguzi wa kutosha na wakunga wa kutosha. Madaktari wasaidizi wanasaidia sana kufanya operation hasa kwa akina mama wajawazito ambao hushindwa kujifungua, wakunga pia ni muhimu sana kwa ajili ya kuzalisha akina mama wajawazito. Akina mama wengi hupoteza maisha kwa kushindwa kujifungua kama vituo vya afya hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu huduma za Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) huduma za Bima ya Afya itakuwa na maana kila kituo cha kutolea huduma kama vile zahanati, vituo vya afya, Hospitali za Wilaya na Mikoa kama vituo hivyo vitakuwa na dawa na vifaa tiba vya kutosha badala ya wanachama wa bima ya afya wataambiwa wanunue dawa katika maduka binafsi.

Mheshimwa Mwenyekiti, kuhusu Bohari ya Dawa (MSD); kwanza ninaipongeza sana Bohari ya Dawa (MSD) kwa kazi nzuri sana ya kusambaza dawa na vifaa tiba katika vituo vya kutolewa huduma za afya, changamoto kubwa katika taasisi hii ni kutokupewa fedha za kutosha kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba ili kusambaza katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya. Ushauri wangu ni kwamba MSD watengewe fedha za kutosha kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa Afya ni muhimu sana hasa katika kusimamia afya ya mazingira na kuzuia magonjwa ya kuambukiza kama vile kipindupindu (cholera), magonjwa ya kuharisha (dysentery),typhoid fever na kadhalika. Ipo haja ya kuimarisha Idara ya Afya Kinga (Preventive Services).

Maafisa wa Afya wakitekeleza majukumu yao vizuri hata magonjwa ya kuambukiza yatapungua. Naomba maelezo kwa nini Maafisa Afya wanahamishiwa Ofisi ya Makamu wa Rais, Idara ya Mazingira? Maafisa wa Afya ni watumishi halali wa Wizara ya Afya na wamesomeshwa na Wizara ya Afya, kwa nini sasa wahamishiwe Ofisi ya Makamu wa Rais –Idara ya Mazingira? Nashauri Maafisa Afya wote warudishwe Wizara ya Afya - Idara ya Kinga na kusambazwa katika Wilaya zote hapa nchini.