Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuitumikia nchi yetu. Mheshimiwa Waziri nikuombe sana ukiangalie kituo cha afya Kitomanga kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, kituo hiki hivi sasa kinafanya kazi kubwa kama hospitali ya Wilaya lakini uwezo wake ni wa kituo cha afya. Changamoto kubwa iliyopo katika kituo kile ni uchache wa vitanda, kutokamilika kwa jengo la x-ray pamoja na kuchakaa kwa gari la wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali sana nakuomba utuokoe kwa kutupatia gari la wagonjwa katika kituo cha afya Kitomanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu vyoo katika shule za msingi. Nakumbuka mwaka jana nilikueleza changamoto ya vyoo iliyopo katika shule nyingi za msingi zilizopo Jimboni kwangu. Changamoto hii zinawaathiri sana wasichana wawapo shuleni. Nakumbuka uliniahidi kutupatia fedha kwa ajili ya kujenga vyoo kadhaa katika baadhi ya shule za msingi ukataja kuwa upo mradi Wizarani kwako ambao ungeweza kutusaidia katika baadhi ya shule. Ahadi yako ile bado hadi sasa hajalitekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu fedha kidogo ya dawa zinazoletwa katika Mkoa wetu wa Lindi. Mheshimiwa Waziri nakuomba uipitie taarifa yako uliyoisoma hapa Bungeni, utagundua kuwa Mkoa wa Lindi umepata asilimia 70 tu ya fedha mliyoitenga mwaka wa fedha 2016/2017 tatizo ni nini? Lindi ni Mkoa ambao wakazi wake wengi ni maskini wenye kipato cha chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu kukosekana kwa Sheria ya Wazee ambayo inapaswa kwenda sambamba na Sera ya Wazee ya mwaka 2003. Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Sheria ili sera hii itungiwe sheria yake?